Na Masanja Mabula -Pemba ..
WAJASIRIAMALI
wa kilimo cha biashara nchini, wameshauriwa kuwa na mawasiliano ya
karibu miongoni mwao, ili kuepusha kulima na kuvuna kilimo cha aina moja
na kukosa soko la uhakika la bidhaa zao.
Ushauri
huo umetolewa, na Mkurugenzi wa Ushirika kutoka Wizara ya Kazi,
Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Khamis Daud Simba,
alipokuwa akizungumza kwenye mafunzo ya kuzijengea uwezo redio jamii
kisiwani Pemba, ili kuandaa vipindi vya kuwaelimisha wananchi juu ya
ujio wa Saccos za wilaya.
Alisema,
wajasiriamali wamekuwa mstari wa mbele kulima kilimo cha mboga mboga
kwa ajili ya biashara, ingawa wamekuwa wakikosa soko la uhakika,
kutokana na kulima na kuvuna kwa pamoja.
Mkurugenzi
huyo alieleza kuwa, kama wakiwa na mawasiliano ya pamoja, watajipangia
kwa kupishana, jinsi ya ukulima kwa kutangulia kundi moja na kisha
jengine kufuata.
“Kama
wajasiriamali wa kilimo wakiwasiliana juu ya kilimo, na kuacha mtindo
wa kulima na kuvuna kwa pamoja, basi soko linaweza kuwa hafifu kwa
wateja kuzidiwa na bidhaa’’,alifafanua.
Katika
hatua nyengine Mkurugenzi huyo, amewataka wananchi waliojiunga kwenye
Saccos ndogo ndogo, kujipanga vyema, ili kuzitumia vyema Saccos za kila
wilaya zao.
Akifungua
mafunzo hayo, Naibu waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Vijana, Wazee, Wanawake
na Watoto Shadya Mohamed Suleiman, amewataka waandishi wa habari
kuwaelimisha wananchi, juu ya ujio wa Saccos za wilaya.
“Nyinyi
waandishi wa habari, tunawategemea sana katika kuwafikia wananchi na
kuwaelimisha kuwa, sasa serikali inataka kutanua wigo wa kuwainua
kiuchumi, kwa kuwepo kwa Saccos ya wilaya’’,alifafanua.
Nae
Naibu Katibu Mkuu, anaeshughulia wanawake na watoto Zanzibar Mauwa
Makame Rajab, alisema redio za jamii zinamchango mkubwa, katika kufikia
malengo ya wanajamii husika.
“Wizara
kwa makusudi, imeamua kuwapa mafunzo ya siku moja ya utayarishaji wa
vipindi vyenye kuelimisha jamii, juu ya ujio wa Saccos za
wilaya”,alifafanua.
Meneja
redio jamii Mkoani Ali Abass Omar, ameahidi kuwa watawaelimisha
wananchi, juu ya azma ya serikali katika kuanzisha Saccos za wilaya.
Hata
hivyo mtangaazaji wa ZBC redio Khadija Kombo Khamis, amepongeza hatua
ya Idara ya vyama vya ushirika kuwashirikisha kikamilifu, ili
kuwaelimisha wananchi.
Idara
ya vyama vya ushirika Zanzibar, inakusudia kuanzisha kwa Saccos za kila
wilaya Unguja Pemba, ili wananchi wawe na mitaji mikubwa, huku
wakizitumia redio jamii za Mkoani na Micheweni kuwaelimisha wananchi
No comments:
Post a Comment