Skip to main content
UJUE MTI WA MAAJABU DUNIANI, UNA ZAIDI YA VIRUTUBISHO 96 KWA AFYA
UJUE MTI WA MAAJABU DUNIANI, UNA ZAIDI YA VIRUTUBISHO 96 KWA AFYA
Mlonge
ni mti ambao umeiteka dunia na kuwa mti wa maajabu duniani kutokana na
ubora wa hali ya juu na kuwa na virutubisho(nutrients) zaidi ya 96,
madini zaidi ya 46 na si hivyo tu bali na kutumika kama zao la chakula,
Dawa, lishe, mboga za majani, juisi, chai na mambo mengine kadha wa
kadha. Mti huu umepewa kipaumbele sana na nchi mbalimbali duniani
ikiwemo Marekani, ufilipino, na hata barani Afrika kama Afrika kusini,
Senegal, Kenya n.k kutokana na faida zake ambazo zinapatikana katika
majani yake, mizizi na hata mbegu zake.
Mlonge unasifika na kupendwa kama zao la chakula, dawa na hata
kibiashara ambalo ni zao la kudumu(permanent) na husitawi na kuota
katika ardhi yoyote ile na katika kila aina ya vipindi vya majira
kutokana na desturi yake ya kuchipua shina juu ya shina na na kukua
ndani ya wiki mbili ambapo mlimaji huanza kuvuna mazao(chakula) na pia
huongezeka kimo wiki, mwezi, mwaka na miaka kutokana kiwango chake
kizuri cha uhifadhi wa maji hali ambayo imewafanya watu mbalimbali
duniani kuuita mti huu kuwa ni mti wa maajabu na jina lingine
liliozoeleka ni Moringa Oleifera. Licha ya
mlonge kuwa bora kwa chakula pia unatoa vitamin A, C, B, E, pamoja na
madini ya Protini, chuma, Magniziam, Nitrojen na mengine mengi pia mti
huu unasaidia kuondoa vitambi, kusafisha macho, dawa ya kusafishia
nywele, kukomaza mifupa na kurekebisha mzunguko wa damu ikiwa ni pamoja
na kusaidia zaidi katika tatizo la shinikizo la damu (BP), Wataalamu
wanasema ukitumia mlonge unakuwa umepata mlo kamili na kupata
virutubisho vyote ambavyo ungepata katika vyakula na matunda mfano
Karoti, Mayai, nyama, mahindi n.k
Kumekuwepo na hali ya sisi binadamu kupuuza baadhi ya miti hata
kuikata ili kutengenezea kuni na hata wengine pia kuchoma mkaa huku
tukisahau umuhimu wa kuwa na miti hii, pia tunashuhudia baadhi ya watoto
wachanga huzaliwa wakiwa na tatizo la utapia mlo, mama pia kukosa
maziwa kumnyonyesha mtoto bila kujua nini tatizo! Wahenga walisema
“Kuzaa mwana si kazi bali kazi ni kumlea huyo mwana” hii inajidhihirisha
bayana kutokana na mti huu wa Mlonge kuwa na madini ya nitrojeni na
chuma ambayo yatamsaidia mama Mjamzito kujenga mifupa ya mtoto tumboni
na pia hata mtoto atakapo zaliwa ataweza kupata maziwa ya kutosha kutoka
kwa mama ili kumnyonyesha vyema na kuwa na afya njema. Mlonge pia
hutibu Bacteria na fangasi, unaweza pia kutengeneza chai ya mlonge ambao
uko katika hali ya unga, pia kupata mafuta kutokana na mbegu zake pia
sabuni kutokana na mlonge kwani hauna kemikali zozote.
Watu mbalimbali duniani wamenufaika na kufanikiwa kiuchumi kwa
kutumia mlonge kulima kama zao la biashara pamoja na chakula na
kuyaendesha maisha yao vyema kama utakavyoona katika vidokezo(links)
hapo chini. Sisi watanzania tunaweza hebu tujiokokoe katika janga la
njaa na umasikini kwa kulithamini zao hili la mlonge kama utajiri wetu
na daktari wa afya yetu hususani katika Maisha yetu hasa kwenye
kipaumbele cha kilimo kwanza. Nina imani mpaka hapo umeufahamu na kuujua
mti wa maajabu duniani na faida zake. Huu ndio mti wa maajabu (Miracle
tree)
Unitaji mlonge 0756 483 174
Comments
Post a Comment