Mwongozo wa Kilimo Bora cha Papai



Utangulizi:
Mapapai ni zao moja kati ya mazao ya matunda yenye vitamini A na madini ya kalsiamu kwa
wingi. Inaamanika asili ya papai, ni huko nchi za Amerka ya kati, (Mexico), ndipo zao ili likasambaa duniani kote. Kwa sasa zao hili hulimwa karibu kila mahali hapa nchini. Papai ni moja ya mazao yenye faida kubwa na yenye soko la uhakika. Ekari moja ya papai ikitunzwa vizuri inaweza kukupatia faida ya zaidi ya milioni 20 kwa kipindi cha miaka 2 hadi 3.
Kuna aina 3 za mbegu za papai.

1. Mbegu za kienyeji (local varieties). hizi ni aina ya papai za kienyeji ambazo, mara nyingi hazifahamiki majina yake. Mbegu zake huwezi zipata kwenye mfumo rasmi wa mbegu (madukani) nk. mara nyingi mbegu hizi hupatikana kwa kuchukua matunda yaliyoiva na kuchukua mbegu zake.. kiswahili cha mtaani husema mbegu za kukamua..
2. Aina za kawaida (open pollinated varieties kwa kifupi OPV). Mfano wake ni kama Calina nk hizi hua na uzao wa kati.
3. Chotara (hybrid). Mfano Malkia F1, Sinta F1, Red royal mk. Hizi hufanya vizuri maeneo mengi.. hua na uzao mkubwa kuliko aina nyingine tulizojifunza hapo juu
MAMBO YA KUZINGATIA WAK ATI WA UZALISHAJI
Ili kupata mazao yenye ubora unaotakiwa ni muhimu kuzingatia kanuni za kilimo bora za uzalishaji
wa mapapai. Ubora wa matunda baada ya kuvunwa hutegemea jinsi yalivyozalishwa. Baadhi
ya kanuni hizo ni kama zifuatazo:
Kuchagua aina bora
Chagua aina bora ya kupanda kulingana na mahitaji ya soko.
Kudhibiti wadudu, magonjwa na magugu
Mapapi hushambuliwa kwa urahisi na magonjwa na wadudu, hivyo ni muhimu kufanya ukaguzi
wa mara kwa mara ili kugundua dalili za mashambulizi.
Endapo kuna dalili za mashambulizi, dhibiti mapema ili kuzalisha mazao bora yanayoweza
kuhifadhiwa kwa muda mrefu.
Pia hakikisha shamba na barabara zake ni safi wakati wote ili kurahisisha uvunaji na
usafirishaji.
Maandalizi kabla ya kuvuna
Kukagua shamba
Kagua shamba kuona kama kuna mapapai yaliyokomaa
Mapapai hukomaa katika kipindi cha miezi minne hadi mitano kutoka maua yanapochanua.
Dalili za mapapai yaliyokomaa
Tunda hubadilika rangi kutoka kijani kibichi na kuwa ya kijani nyepesi hadi manjano.
Kuandaa vifaa vya kuvunia, kufungashia na kusafirishia
Vifaa vya kuvunia
Vichumio
Mifuko
Ngazi
Vifaa vya kufungashia
Makasha ya mbao/ plasitiki au makaratasi magumu
Vyombo vya kusafirishia
Mikokoteni
Magari
Matela ya matrekta
Kuvuna
Uvunaji bora wa mapapai ni wa kutumia mikono ambapo tunda huchumwa kwa mkono au kwa kutumia vichumio maalumu.
Vuna mapapai yaliyokomaa tu
Vuna mapapai pamoja na vikonyo vyake
Vuna kwa uangalifu ili kuepuka kudondosha matunda
Matunda yakidondoka, huchubuka, hupasuka au hupondeka hivyo husababisha upotevu.
W eka mapapai kivulini mara baada ya kuvuna
Kuchambua, Kusafisha na Kupanga Madaraja
Ni muhimu kuchambua mapapai ili kutenga yaliyooza, kupasuka na yenye dalili za magonjwa au kubonyea. Lengo la kuchambua ni kupata matunda yenye ubora kulingana na matumizi , kwa mfano kusindika, kuuza au kusafirisha.
Matunda yaliyooza na yenye wadudu ni vyema yafukiwe ili kuangamiza wadudu waharibifu
na vimelea vya magonjwa, na pia kuzuia kuenea kwa wadudu na magonjwa hayo.
Matunda yaliyopasuka, kubonyea au kuchubuka kidogo yatumike haraka kwa kuliwa.
Matunda mazuri ambayo hayajapata madhara yoyote yatumike kwa ajili ya kusindika, kuliwa, kuuzwa au kusafirishwa.

Comments

Popular Posts