Hali ya chakula nchini kuelekea mwaka 2017
1. Hali ya Chakula
Hali ya chakula mwaka 2016/2017
ni ya kuridhisha kutokana na mavuno yaliyopatikana msimu wa kilimo wa
2015/2016. Tathmini ya awali (Preliminary Forecast) ya uzalishaji wa mazao ya
chakula iliyofanyika mwezi Julai 2016, nchi inajitosheleza kwa chakula kwa
viwango vya utoshelevu vya asilimia 123. Kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara
Mikoa 11 ilibainika kuwa na viwango vya ziada vya chakula mikoa 12 ina hali ya
utoshelevu na mikoa 2 ina uhaba wa chakula.
Katika mikoa 15 ilibainika kuwa na maeneo yenye uhaba wa chakula katika
Halmashauri 43 hatahivyo mkoa wa Kagera na lamashauri 3 za mkoa huo zimekuwa na
maeneo tete baadaye kutokana na athari za tetemeko la ardhi pamoja na ukame
ulioathiri mazao kwa kiasi kikubwa.Kwa ujumla hali ya chakula inaridhisha
ukilinganishwa na mwaka uliopita kwa kuwa kulikuwa na jumla ya Halmashauri 69
zilizokuwa zimebainika kuwa na maeneo yenye uhaba wa chakula katika mwaka
uliopita.
2. Uzalishaji wa Chakula
Taarifa ya Tathmini ya awali
(Preliminary Forecast) na uzalishaji wa mazao ya chakula kwa mwaka 2015/16
inaonesha kuwa kitaifa, uzalishaji wa chakula utafikia tani 16,172,841 za
chakula (kwa mlinganisho wa nafaka – Grain Equivalent), ambapo tani 9,457,108
ni za mazao ya nafaka na tani 6,715,733 ni za mazao yasiyo nafaka. Mahitaji ya
chakula kwa mwaka 2016/17, tunahitaji tani 13,159,326 ambapo tani 8,355,767 ni
za mazao ya nafaka na tani 4,803,560 ni za mazao yasiyo nafaka.
Uzalishaji wa zao la mahindi
katika mwaka 2015/2016 ulikuwa tani 6,148,699 ambapo mahitaji kwa mwaka
2016/2017 ni tani 5,202,415. Hivyo, kulikuwa na ziada ya tani 946,284 za
mahindi kwa kiwango cha utoshelevu wa asilimia 118. Kwa upande wa uzalishaji wa
mchele, jumla ya tani 2,229,071 zilizalishwa kwa mwaka 2015/2016 ambapo
mahitaji ya zao hilo kwa mwaka 2016/2017 ni tani 976,925. Hivyo, kulikuwa na
ziada ya tani 1,252,146 za mchele kwa kiwango cha utoshelevu wa asilimia 228.
3. Hifadhi ya Chakula ya Taifa
Serikali kupitia Wakala wa Taifa
wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) kwa mwaka wa fedha 2016/2017 umepanga kununua
jumla ya tani 100,000 za chakula. Hadi kufikia tarehe 24 Novemba 2016, Wakala
umenunua jumla ya tani 61,145.245 za chakula sawa na asilimia 61 ya lengo
ililojiwekea. Kati ya kiasi hicho, tani 38,132.389 zimenunuliwa kupitia vituo
vya ununuzi na tani 23,012.906 kupitia vikundi vya wakulima. Hata hivyo, hadi
kufikia tarehe 24 Novemba, 2016 Wakala umetoa jumla ya tani 20,048.521 za
chakula. Aidha, hadi kufikia tarehe 26 Disemba, 2016 Wakala una akiba ya tani
90,716.798 za chakula.
4. Matarajio ya Hali ya Chakula
Tanapoanza mwaka 2017,
tunatarajia hali ya chakula kuendelea kuwa ya kuridhisha kutokana na mavuno ya
msimu uliopita wa 2015/2016. Bei ya chakula husuani mahindi katika kipindi hiki
imepanda kidogo ukilinganisha na bei za mwaka jana mwezi kama huu. Mwenendo wa
kupanda kwa bei ya mazao unatokana na kupungua kwa uingizaji wa mazao sokoni
ambayo ni hali ya kawaida kila mwaka. Bei ya mchele sokoni bado ni ya
kuridhisha.
Mvua za vuli zilichelewa kuanza na zimenyesha chini ya kiwango na kwa
mtawanyiko usioridhisha katika maeneo
yanayopata mvua mara mbili kwa mwaka. Uzalishaji unaotokana na mvua za vuli
huwa unachangia takribani kati ya asilimia
17 hadi 20 ya chakula nchini. Aidha, maeneo yanayopata mvua mara moja kwa mwaka
(mvua za msimu) mvua zimeanza pia kwa kuchelewa na za chini ya kiwango. Hali
hiyo, kwa kiasi fulani inazidi kuathiri uingizaji mazao ya chakula kwa wingi sokoni na hasa mahindi kutokana na
wafanyabiashara kuhodhi mazao hayo wakiwa na mategemeo ya bei kupanda baada ya
taarifa za hali ya unyeshaji mvua kuonyesha kuwa mvua zitakuwa chini ya kiwango
na hivyo uzalishaji unategemewa kutokuwa wa kuridhisha.Mabadiliko ya tabia nchi
kwa kiasi kikubwa yamechangia mvua kunyesha chini ya kiwango na kwa mtawanyiko
mbaya.
Wizara inaendelea kuwasiliana na
mikoa ili kufuatilia kwa karibu hali ya upatikanaji wa chakula pamoja na bei, mwenendo wa mvua na hali
ya mazao mashambani.Taarifa zinazopatikana zitaisaidia Serikali na kuchukua hatua stahiki kulingana na hali itakayojitokeza. Aidha,
tathmini ya kina ya hali ya chakula na Lishe inatarajiwa kufanyika katika
maeneo yenye hali tete mwanzoni mwa mwezi Januari 2017 ili kubaini idadi ya
watu walioathirika na mahitaji ya chakula na mbegu.
5. Ushauri
- Wafanyabiashara watumie fursa ya kuwa na bei nzuri ya mazao kutoa akiba ya mazao waliyoyahifadhikatika maghaliaa yao na kuyaingiza katika soko.
- Wakulimawatumie mvua zinazonyesha kupanda mazao yanastahimili mvua kidogo na yanayokomaa mapema.
- Wataalam wa kilimo wanatakiwa kuendelea kutoa ushauri kwa wakulima juu ya mazao yanayofaa katika maeneo yao ili kutumia vizuri mvua zinazoendelea kunyesha.
- , Wananchi kote nchini wanatahadharishwa juu ya kuzingatia hifadhi ya mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambayo yanaathiri kwa kiwango kikubwa mzunguko na upatikanaji wa mvua zinazotosheleza uzalishaji wa mazao hapa nchini.
Kiambatisho
1a: Mwenendo wa bei za mazao ya chakula, kwa miaka ya 2002 hadi 2016
|
|||||||||||||
(Bei
(TSh) kwa Gunia la Kilo 100)
|
|||||||||||||
|
MWEZI
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
||
ZAO
|
|
JAN
|
FEB
|
MAR
|
APR
|
MEI
|
JUN
|
JUL
|
AUG
|
SEP
|
OKT
|
NOV
|
DEC
|
Mahindi
|
2002
|
14,363
|
14,716
|
15,267
|
14,055
|
10,987
|
9,035
|
9,190
|
9,237
|
10,005
|
11,262
|
11,446
|
11,586
|
|
2003
|
13,471
|
12,413
|
13,028
|
14,089
|
14,333
|
15,025
|
16,347
|
17,215
|
17,323
|
17,713
|
18,678
|
21,804
|
|
2004
|
25,260
|
25,957
|
25,816
|
21,154
|
15,855
|
13,400
|
13,997
|
16,069
|
16,239
|
16,440
|
16,652
|
16,467
|
|
2005
|
16,221
|
14,298
|
14,656
|
15,500
|
16,020
|
17,072
|
16,839
|
16,372
|
16,402
|
16,364
|
18,763
|
22,099
|
|
2006
|
29,945
|
30,594
|
32,046
|
33,139
|
30,406
|
25,973
|
22,112
|
20,554
|
19,679
|
19,460
|
18,789
|
18,095
|
|
2007
|
19,104
|
18,283
|
17,815
|
17,026
|
17,371
|
16,882
|
18,241
|
19,528
|
21,802
|
24,394
|
25,468
|
28,281
|
|
2008
|
32,065
|
31,181
|
35,458
|
32,798
|
30,090
|
28,194
|
28,628
|
28,867
|
28,792
|
30,927
|
32,391
|
35,029
|
|
2009
|
36,612
|
39,314
|
38,022
|
35,959
|
35,005
|
35,245
|
34,128
|
32,481
|
36,801
|
38,439
|
40,930
|
43,841
|
|
2010
|
46,111
|
46,472
|
41,426
|
33,864
|
29,542
|
27,530
|
27,745
|
28,259
|
28,988
|
30,217
|
32,050
|
33,695
|
|
2011
|
35,133
|
37,531
|
40,740
|
43,666
|
42,265
|
43,326
|
44,524
|
42,246
|
42,227
|
41,492
|
42,242
|
42,976
|
|
2012
|
44,437
|
42,388
|
43,270
|
46,751
|
51,185
|
50,378
|
50,165
|
50,487
|
54,291
|
58,120
|
65,498
|
56,318
|
|
2013
|
|
77,416
|
73,192
|
64,842
|
65,431
|
49,096
|
49,967
|
52,554
|
53,539
|
53,686
|
53,826
|
55,674
|
|
2014
|
|
54,547
|
51,855
|
49,876
|
47,583
|
47,681
|
44,642
|
41,313
|
40,602
|
39,510
|
38,243
|
38,470
|
|
2015
|
38,232
|
37,355
|
39,491
|
47,702
|
47,042
|
48,025
|
52,219
|
56,318
|
57,717
|
57,756
|
63,774
|
65,104
|
|
2016
|
67,048
|
67,326
|
63,912
|
57,431
|
55,976
|
53,986
|
57,011
|
55,571
|
56,312
|
63,133
|
72,133
|
|
Kiambatisho
1b: Mwenendo wa bei ya mahindi
Comments
Post a Comment