Matumizi ya Mbolea
Matumizi ya rutuba kwenye udongo
} Mimea huchukua /huondoa virutubisho kutoka kwenye udongo kupitia
kwenye mizizi.
} Virutubisho vinavyotumika na nafaka kama (ngano, mahindi, mpunga,
n.k) inageuzwa kuwa punje na sehemu kwenye masalia ya mimea.
} Kwa upande wa mahindi ,kwa kila kilogramu 1000 ya mazao
yanayozalishwa ,Kilogramu 35 za virutubisho zinakuwepo kwenye mazao na
kilogramu 37 kwenye masalia ya
mimea.Jumla ya kilogramu 72 za virutubisho zinakuwa zimetoweka.
} Iwapo kwenye hekta moja umevuna tani 4 =kilogramu 4000, kiasi cha
kilogramu 288 ya virutubisho itakuwa imeondolewa kutoka kwenye udongo.
} Kama hivi virutubisho havitarudishwa, rutuba ya udongo itapungua
.Kwa miaka kadha wa kadha, mavuno kutoka kwenye udongo wa aina hiyo inashuka.
} Kwa udongo kubaki na rutuba, ni vizuri kurudisha virutubisho vilivyo
potea wakati wa mavuno ya mazao.
Kutoka: IFDC: Estimated removal of
nutrients from the soil by Grains (kg nutrients/ Mt grain harvested)
Mimea
|
Nitrojeni
(N)
|
Fosforasi
(P2O5)
|
Potasiamu
(K2O)
|
Jumla
|
Mahindi
|
18
|
10
|
7
|
35
|
Ngano
|
20
|
8
|
5
|
33
|
Mpunga
|
14
|
6
|
4
|
24
|
Kutoka: IFDC: Estimated removal of
nutrients from the soil by
Residue (kg nutrients/ Mt straw harvested)
Mimea
|
Nitrojeni
(N)
|
Fosforasi
(P2O5)
|
Potasiamu
(K2O)
|
Jumla
|
Mahindi
|
10
|
6
|
21
|
37
|
Ngano
|
6
|
3
|
22
|
31
|
Mpunga
|
9
|
2
|
24
|
35
|
Virutubisho ni nini?
} Mimea inahitaji virutubisho kumi na sita ili kukua na kutoa maua na
mazao mazuri.
} Virutubisho hutumika kama lishe ya mimea.
} Virutubisho vitatu hutoka hewani mambavyo ni: kaboni, oxijeni na
hydrojeni.—Ikichangia asilimia 93 ya mahitaji ya mmea.
} Wakati virutubisho vitatu hutokana na hewa na maji .
} vingine kumi na tatu hupatikani kupitia udongoni.Hupatikana kupitia
mizizi na kutumika na mimea.
Madaraja ya virutubisho vya mimea
} Kwa kuzingatia kazi zake na kiwango kinachohitajika na mimea kwa
ukuaji kumetokea madaraja yafuatayo:
- Virutubisho vya msingi au vinavyohitajika kwa wingi
} Nitrojeni (N), Fosforasi (P), Na potasiamu (K) ndivyo vinahitajika
mno na mimea kwa ukuaji na kwa kiwango kikubwa.
- Virutubisho vinavyo hitajika kwa kiasi
} Kalsiamu (Ca), salfa (S), and magnesiamu (Mg) huhitajika kwa kiasi
kidogo na mimea lakini vinaumuhimu mkubwa.
3. Virutubisho vinavyo hitajika kwa
kiwango kidogo
} Virutubisho saba vilivyobaki ambavyo ni: Chuma (Fe), Kopa (Cu),
zinki (Zn), boron (B), manganese (Mn), clorini (Cl), and molybdenum (Mo)
huhitajika kwa kiwango kidogo sana.
Dalili kutokana na ukosekanaji wa
vitutubisho Dalili kutokana na ukosekanaji wa vitutubisho
Virutubisho vya msingi
} Nitrogen (N), phosphorus (P), and potassium (K) ni vya aina tatu.
Kutokana na makubaliano ya vigezo vilivyowekwa
na viwanda vya mbolea, virutubisho vya muhimu /msingi vimekubalika kama; N
(nitrogen), P2O5 (or phosphorus pentoxide for phosphorus), and K2O (or
potassium oxide for potassium
1.
Nitrogen
2.
Nitrojeni ndio kirutubisho cha
muhimu kwa aina kubwa ya udongo unaonjesha mapungufu.
3.
Ijapokuwa Nitrojeni inahitajika
katika ukuaji wa awali wa mimea ,inahitajika kwa kiwango kikubwa wiki ya 3-4
kutoka zao kuota haswa kwa mazao ya nafaka kama ngano,mahindi ,mpunga n.k.
4.
Nyongeza huwekwa baadae wakati
mimea inapacha ,kutoa maua au karibu na kukomaa.
5.
Kwa hiyo Nitrojeni huwekwa kama
mara 2-3 kwenye mimea
Dalili za mapungufu
ya Nitrojeni
} Kama nitrojeni imekosekane kwenye udongo:
} Ukuaji wa mmea huwa taratibu.
} Mmea hudumaa na majani kuwa ya njano.
} Mmea hukomaa haraka kupunguza mavuno.
} Upungufu wa Nitrojeni
} Mapungufu ya nitrojeni hupatikana karibu kila eneo lakini zaidi
kwenye udongo wa kichanga, udongo wenye kiwango kidogo cha mboji, au udongo
uliolimwa mfululizo kwa miaka mingi.
} Aina ya mbolea inayotumika sana kusambaza nitrojeni ni mbolea ya
Urea,SA,CAN
Mbolea
|
Virutubisho %
N:P:K
|
Hutumika
haswa
|
Urea
|
46:0:0
|
Kukuzia
|
Calcium
Ammonium Nitrate(CAN)
|
27:0:0
|
Kukuzia
|
Sulphate of
Ammonia(SA)
|
21:0:0
|
Kukuzia
|
Di -ammonia
Phosphate (DAP)
|
18:46:0
|
Kukuzia
|
N:P:K
|
17:17:17,20:10:10
|
Kukuzia
|
2. Fosforasi
} Fosforasi hupitia kwa mmea kwa kutumia mbolea za fosfeti,mara nyingi
hutumika kupandia.
} Fosfati ni muhimu sana
kipindi cha awali cha ukuaji wa mmea kwa
kuuwezesha mmea kuwa na mizizi mingi na kuwa na nguvu ya kuushikilia mmea
kwenye udongo.
} Mizizi yenye afya huufanya mmea kupata vitutubisho kwenye udongo.
Dalili za mapungufu
ya fosforasi
} Upungufu wa Fosforasi Huonekana haswa kwenye udongo wenye tindikali
au ulio na kalsiuamu /chokaa kwa wingi.
} Mapungufu ya fosforasi kwenye udongo huufanya mmea kuwa :
} Dhaifu kutengeneza mizizi.
} Kuanguka kwa mmea.
} Kudumaa kwa mmea na mavuno kidogo.
} Mfano wa mbolea zenye Fosforasi ni: SSP (0-16-0),TSP (0-46-0),DAP
(18-46-0)
3.
Potasiamu
} Potasiamu ni aina ya tatu ya kirutubisho cha msingi kinachohitajika
na mimea.,barafu ,wadudu na magonjwa na kusaidia usafirishaji wa virutubisho
vingine kuanzia kwenye mizizi hadi sehemu nyingine ya mimea.
} Inasaidia kujaza punje,mbegu.
} Mbolea zote zinazosambaza Potasiamu hutumika kupandia ila kwenye
udongo wa kichanga inashauriwa kuwekwa mara mbili wakati wa kukuzia.
Dalili za mapungufu
ya potasiamu
} Majani huonjesha dalili ya kama kuungua kwenye njia ya jani na
kuendelea.
} Kwa lugha ya kitaalamu huitwa “chlorosis.”
} Mimea inakuwa dhaifu kwa mashambulizi ya magonjwa.
} Salfa inahusika kwenye protini ya mmea
,husaidia vimengényo na vitamini vinavyohitajika kwenye kutengeneza ukijani
unaosaidia kuakisi mwanga wa jua
.
} Sulfur inapatikana kwenye vitu vingi Kama vile gypsum na mbolea kama
ammonium sulfate, SSP and TSP.
Matumizi ya mbolea
Asilia/Mboji
} Mboji ni urutubishaji wa asili ambao hujirudia wenyewe kwa mtindo wa
kuoza. Utengenezaji wa mboji ni njia ya
kurudisha rutuba ya asili kwenye udongo kwa njia ya kuozesha vitu.
} Matokeo yake ya mwisho ni kutoa mbolea asili ambayo ni rahisi
kutengeneza, na ambayo ina virutubisho vingi bila gharama
} Mboji huwa ni faida kutokana na uozaji wa asili ambao hutokea kwenye
vitu vyote vyenye uhai.
} Vitu vyenye uhai ni kama vile majani, miti na mabaki ya
vyakula.wakati wa uozaji vitu hivi hugeuka na kuwa rutuba inayorudia kwenye
udongo
} Udongo hupoteza virutubisho baada ya kutumika sana .
} Matumizi ya mbolea za asili nayo ni mazuri katika kuendeleza udongo
kwa ajili ya ukulima.
} Pia mbolea za asili/mboji husaidia kuzuia mmomonyoko wa ardhi
} Inaruhusu mmea kupata rutuba kwa urahisi kutoka kwenye udongo.
} Pia hufanya mmea usiwe dhaifu kwahiyo huzuia wadudu waharibifu
kushambulia mmea.
} Mboji hutoa virutubisho kwa muda mrefu kwasababu ya uendeleaji wa
kuoza polepole.
} Madini yaliyopo katika mboji husaidia kuyeyusha madini mengine
yaliyo kwenye udongo,
} Hufanya madini yenye rutuba yapatikane zaidi kwa mimea. Madini hayo
huimarisha sehemu laini za mizizi na hivyo kuipa mizizi uimara wa kuweza kupata
maji na virutubisho kwa njia ya mizizi
Hitimisho
} Mbolea ni kitu muhimu sana katika udongo kwa sababu mazao huitaji
virutubisho katika udongo na baada ya udongo kutumika kwa muda mrefu ,
virutubisho hupotea.
} Kuvirudisha virutubisho, mbolea inahitajika inaweza ikawa ya
chumvichumvi au ya asili hii hutegemea na udongo uliopo katika sehemu hiyo.
} Kila sehemu ina udongo wa aina yake na unahitaji virutubisho vya
aina yake kwa wingi au kiwango kidogo.
} Kwa hiyo uwekaji wa mbolea katika udongo lazima utumie utaalamu
ambao mkulima amepata kutoka kwa wataalamu wa kilimo au uzoefu.