Matumizi sahihi ya viatilifu

Kila mwaka, viatilifu vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya dola za kimarekani 38
huongezwa katika mazingira kwa makusudi ikiwa ni matumizi ya kawaida ya
binadamu. Katika siku za hivi karibuni, tanzania imekua moja kati ya watumiaji
wanaokua wa viatilifu.

Sehemu kubwa ya viatilifu hivi ni sumu za viwango vya juu na vina madhara ama ya papo kwa papo ama ya muda mrefu kwa afya ya binadamu, wanyama, mimea na wadudu.
Madhara ya muda mrefu ni pamoja na saratani, matatizo ya uzazi, kuharibika kwa homoni na uharibifu wa kinga ya mwili. Madhara haya hutokana na kutumia viatilifu hivi
moja kwa moja, kuvuta wakati wa kupulizia, kuosha nguo zenye sumu baada ya kazi
na kutunza viatilifu katika nyumba za kuishi.


Namna ya kutumia viatilifu kwa usahihi na usalama
1) 
Vaa mavazi sahihi ya kukukinga
Watu wanaofanya kazi ya kupuliza ama kunyunyiza
sawa mashambani ama katika sehemu nyingine wapo katika hatari ya kugusa, kuvuta
hewa, ama kula sumu kwa bahati mbaya ama kwa kuto kujua.
Mavazi yenye kukinga mwili yatumike ilu
kumuepusha mtumiaji wa viatilifu kuathirika na sumu.
Mavazi hayo ni pamoja na:
·        Kofia
·        Shati la mikono mirefu
·        Suruali
·        Buti (gunboot)
·        Soksi na glovu
·        Miwani
·        Kifaa cha kukinga pua
2)    Zuia watu na wanyama kuingia eneo lililopuliziwa viatilifu baada tu ya kutumia
viatilifu
Taasisi ya kulinda mazingira (EPA) imeweka muda kwa kila kiatilifu ambapo binadamu na
wanyama wanaweza kuingia katika eneo lililopuliziwa kwa usalama. Muda wa
kungoja unategemea aina ya sumu iliyotumika.
Ni vema shamba likipuliziwa sumu liwekewe alama ama ishara inayoonesha hakuna
kuingia shambani. 
Kwa kawaida, usiingie shambani wakati majani bado yamelowa sumu japo zipo baadhi ya sumu ambazo hata kama majani yamekausha sumu hutaruhusiwa kuingia.
NB: Taasisi ya kulinda mazingira =The Environmental Protection Agency (EPA)
3) 
Tumia kiatilifu sahihi kwa kupambana na kisumbufu vilivyopo
Visumbufu vipo vya aina mbalimbali kama vile wadudu, fangasi, magugu, wanyama (kama
panya) hivyo ni muhimu kufahamu sumu zipi ni maalumu kwa kundi lipi la
visumbufu. Mfano, kutumia dawa ya wadudu kuangamiza magugu hakutaleta matokeo
kabisa badala yake kutasababisha sumu kutapakaa katika mazingira.
4)    Tumia kiasi sahihi cha sumu
Katika vibandiko (lebo) za viatilifu, watengenezaji hutaja kipimo cha sumu inayotakiwa
kwa ajili ya kuangamiza visumbufu. Mfano, tumia mililita 10 za dawa kwa lita
moja ya maji endapo majani ni machanga na tumia mililita  15 za dawa kwa kila lita ya maji endapo majani yamekaribia kuchanua.
5)    Tumia sumu yako katika mazingira sahihi
Mazingira yanaweza kusababisha sumu inayotumika kuleta madhara. Sma kibandiko cha dawa na utapata maelezo ya katika mazingira gani sumu hiyo inaweza kutumika kwa usalama zaidi. Mfano, usinyunyize sumu wakati wa upepo mkali maana upepo huweza
kuhamisha sumu na kuipeleka mahali kusiko kusudiwa. Pia sumu isitumike wakati
wa joto kali kama vile mchana kwani joto kali huweza kusababisha sumu kuvukizwa
kwa urahisi hivyo kuisambaza katika hewa.
6)    Tumia njia na kifaa sahihi katika kutumia sumu
Vipo vifaa mbalimbali vinavyotumika katika kusambaza viatilifu katika mashamba ama
maeneo lengwa. Watengenezaji wa sumu husika hutoa maelekezo ya namna na vifaa
sahihi vya kutumia. Mfano, changanya na maji safi na nyunyiza au usichanganye
na kitu chochote, itumike kama ilivyo kwa kunyunyiza katika mazao.


Wednesday, October 5, 2016

Uzalishaji wa vitunguu wenye tija, udhibiti wa Wadudu na Magonjwa ya Vitunguu

Zao la vitunguu hulimwa duniani kote kwa ajili ya kutumika kama kiungo cha chakula. Kila familia angalau hutumia kitunguu mara moja klia siku katika chakula chao. Vitunguu hutumika kama dawa katika baadhi ya jamii na wataalamu wanasema hupunguza shinikizo la juu la damu na kupunguza matatizo mengine ya moyo.

Ili uweze kuzalisha mazao ya jamii ya kabichi unahitaji vitu vifuatavyo:

i) Ardhi yenye rutuba.

ii) Mbegu bora ya vitunguu; k.m Red Creole kutoka ktk chanzo cha kuaminika

iii)  Uwezekano wa kupata maji.

iv)  Dawa za kudhibiti magugu, wadudu na magonjwa.
Uchaguzi wa mbegu bora
Mbegu bora ichaguliwe kwa kuzingatia sifa zifuatazo:

1)     Iwe na ustahimilivu dhidi ya magonjwa na wadudu.

2)     Yenye kutoa mavuno mengi.

3)      Inayokomaa mapema ilu kuwahi soko.

4)     Inayoendana na hali ya hewa ya eneo shamba lilipo.

Uchaguzi wa eneo kwa ajili ya kitalu na shamba:
Udongo – vitunguu ni zao la kina kifupi, udongo uwe laini na usio na mawe wala mabonge ili kuruhusu ukuaji wa kitunguu. pH ya 6-7 na usiotuamisha maji.

 Hali ya hewa: joto la sentigredi 15 – 25

Kupanda moja kwa moja shambani
Ingawa zipo baadhi ya faida za kupanda mbegu za vitunguu moja moja kwa moja shambani (direct seeding) kama kuepuka usumbufu wa kutunza kitalu, njia hii sio maarufu sana miongoni mwa wakulima ukilinganisha na ile ya kutumia kitalu. 
Miche ya vitunguu itakua tayari kwa kupandikizwa kati ya wiki 6 hadi 8 baada ya kupanda kitalu. Wakati wa kupandikiza, itawanye mizizi sawasawa kadri ilivyojipanga katika shina kabla ya kufukia na kushindilia kiasi.
Muhimu; wiki mbili kabla ya kuhamisha miche kutoka kwenye kitalu kwenda kuipandikiza shambani, unatakiwa kuipa miche mazingira halisi ya shambani kwamfano kupunguza kiwango cha maji na kuiondolea kivuli. Hii husaidia kupunguza uwezekano wa miche kufa pindi inapo amishiwa kwenye mazingira mapya ya shamba.

Wadudu waharibifu wa vitunguu
Jina la mdudu
Thiripi (Thrips): Wadudu hawa hukaa kwenye jani sehemu inayokutana na shina. Wadudu hawa hufyonza maji kwenye majani ya vitunguu na kusababisha majani kuwa na doti nyeupe. Husababisha vitunguu kudumaa hivyo kuathiri ukuaji wake jambo ambalo huathiri mavuno pia.
Thrips huudhibitiwa kwa kunyunyuzia dawa iitwayo Protrin 60 EC.
Kimamba: Wadudu hawa hufyonza maji kwenye vitunguu, na kusambaza ugonjwa wa virusi. Husababisha kudumaa kwa vitunguu. Wadudu hawa ni hatari zaidi kwa kuwa husambaza virusi vinavyoingia hadi kwenye mbegu.
Wadudu hawa huthibitiwa kwa kunynyuzia dawa Metakan super 350 SE


Sota (Cutworms): Sota au viwavi wa nondo wanasababisha uharibifu mkubwa. Viwavi wanakata mashina ya miche michanga sehemu ya chini ya shina juu ya ardhi. Sota wanapendelea kula wakati wa usiku na mchana kujificha kwenye ardhi karibu sana na sehemu waliokata shina. Uharibifu huu unapunguza sana idadi ya mimea shambani na kuleta upungufu wa mazao.
Wadudu hawa wanadhibitiwa kwa kupulizia dawa kama; PROTRIN 60 EC, Agromectin 1.8 EC ambayo hutumika ndani ya wiki 0-7 na Metakan super 350 EC nayo hutumika ndani ya wiki 8-20.
Utitiri wekundu (Red spider mites)
Hawa ni wadudu wadogo sana, ambao wanajificha upande wa chini wa majani. Wanafyonza maji maji kwenye majani na kusababisha majani kuwa na rangi nyeupe. Wadudu hawa wanatengeneza utando mweupe kuzunguka majani na mashina. Mmea unashindwa kutengeneza chakula na baadaye inakufa.
Njia ya kudhibiti:
kupulizia dawa za wadudu AGROMECTINE 1.8 EC.
 Vipekecha majani (leaf miner)
Hawa ni aina ya inzi wadogo, ambao viwavi wake wanashambulia majani, kwa kupekecha na kutengeneza mitandao wa mitaro kwenye majani. Viwavi wanashambulia majani na kusababisha majani kukauka. Upungufu mkubwa wa mazao hutokea.
Njia ya dhibiti:
kupulizia dawa ya wadudu kama AGROMETHRIN 10 EC 
kuteketeza masalia ya mazao
kutumia mzunguko wa mazao                    

Magonjwa ya vitunguu
Ugonjwa
Dalili za ugonjwa ni:-
Picha
Baka zambarau (Puple Blotch)
Ungonjwa huu unasababishwa na kuvu (fangasi). Chanzo kikubwa cha ugonjwa ni mbegu zenye ugonjwa. Pia ugonjwa unajitokeza wakati kuna ukungu na unyevunyevu mwingi hewani hasa wakati wa masika.
Kiasi cha 60-80 % ya mazao yanaweza kupotea kama ugonjwa hautadhibitiwa.
ü madoa meupe yaliyodidimia kwenye majani na mashina
ü rangi ya zambarau kuwepo katikati ya doa jeupe.
ü majani kuanguka
Kinyausi (Damping – off)
Ugonjwa huu unasababishwa na fangasi na kuenezwa na udongo, mbegu na masalia ya mazao. Ugonjwa unajitokeza hasa kitaluni ikiwa hali ya hewa ina unyevunyevu na udongo una maji maji.
Kudhibiti: mbegu ziwe safi na ziwekwe dawa ya  AGROZEB 80WP
ü mbegu kuoza kabla ya kuota na kunyauka kwa miche baada ya kuota
Virusi njano vya vitunguu (Onion yellow Dwarf virus)
Ugonjwa huu unasababishwa na virusi na kuenezwa na wadudu aina ya vidukari (wadudu -mafuta).
Kudhibiti ugonjwa huu ni:-
Kutumia mbegu safi
Kuweka shamba katika hali ya usafi
Tumia PROTRIN kuua Wadudu wanaosambaza ugonjwa
Mistari ya rangi ya manjano kwenye majani.
Kujikunja kwa majani
Majani kugeuka rangi ya manjano na kuanguka
Mimea mzima kudumaa, kujikunja na kufa.
asteryellows1_600px.jpg
Ukungu mweusi
Onion Black Mold
Kisababishi: Aspergillus niger
Maranyingi hutokea endapo joto litakua kali.
Kudhibiti: mbegu ziwe safi na ziwekwe dawa ya  AGROZEB 80WP
Agromenol 250EC
Utando mweusi katika gamba la kitunguu.
Kuoza shingo na kirungu
Onion Botrytis Neck and Bulb Rot
Kisababishi : Botrytis allii
Japo Ugonjwa huu huonekana wakati vitunguu vimehifadhiwa, maambukizi huanzia shambani.
Tumia Agromenol 250EC
Kudumaa
Sehemu zilizoathirika hukauka na kufa.
Gamba gumu katika shingo ya kitunguu.
Ubwiri unyoya
Onion Downy Mildew
Kisababishi: Peronospora destructor
Kudhibiti: Meronil 720 EC, rudia kila baada ya siku 7
Manyoya ya kijivu-meupe katika majani ya umri mkubwa.
Kutu
Kisababishi: Puccinia porri
Tumia Agromenol 250EC, Meronil 720 EC, Sipron Star 330 EC
Majani yalioathirika huwa na madoa ya rangi ya machungwa
Baadaye hugeuka na kuwa meusi
Majani yaliyoathirika sana huwa ya njano na hatimaye hufa.

ü  kutumia mzunguko wa mazao
ü  kusia mbegu kwa nafasi za kutosha
ü  kuepukana na kubananisha miche kitaluni
ü  Kuepukanana na kumwagilia maji wakati wa jua kali au wakati kuna ukungu.
ü  kupanda mbegu safi
ü  kupanda vitunguu kwa kutumia mzunguko wa mazao
ü  kuteketeza msalii ya vitunguu baada ya kuvuna

Comments

Popular Posts