Sasa Tanzania imehamasika na kilimo cha vitalu bandani
(Green house farming) baada ya Mtaalamu na Mshauri (Expert) wa masuala
ya kilimo kupatikana na kusema yuko tayari sasa kushirikiana na
watanzania katika kilimo hiki ikiwemo kutoa ushauri wa kitaalamu na
elimu juu ya kilimo.
Akizungumza na tovuti hii, Bw.Daudi Ally Kambanyuma ambaye ni
mwalimu, mshauri, Msomi na mtaalamu wa masuala ya kilimo ambaye ana
uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika masuala ya kilimo na pia ni Mkuu wa
shule ya Sekondari Chita iliyopo wilaya ya Kilombero mkoani Morogoro.
Katika mahojiano na tovuti hii Mwl. Kambanyumba aligusia masuala ya
upandaji na matatizo ya wadudu kuharibu mazao kama changamoto inayo
wakumba wakulima wengi wa vitalu na kuelezea kazi yake maalumu ya kutoa
ushauri kwa wakulima huku akibainisha uzoefu wa utaalamu wake na maeneo
mbalimbali aliyofanya kazi hiyo na jinsi wakulima wa mazao hayo
walivyonufaika. “Sasa ni wakati wetu watanzania kuamka na kuwekeza
katika kilimo cha vitalu bandani maana ardhi tunayo na yenye rutuba,
Suala la Mazao ya baadhi ya wakulima kuharibika yanatokana na wakulima
kutopata wataalamu ambao watafanya tafiti za uchambuzi wa udongo (Soil
Analysis) wa eneo husika hatua ambayo ni ya kwanza kabisa inayokupa
uhakika wa unacho panda, Nimefanya kazi hii kwa muda mrefu na changamoto
zake siku zote ni hii ya wakulima kutozingatia hili” alisema Mwl.
Kambanyuma.
Aidha Mwl. Kamba nyuma amekuwa akifanya kazi za kitaalamu na ushauri wa kilimo na taasisi na mashirika mbalimbali kama Rack Farm, Intermon oxfarm Msowero na Lupalilo Ventures Ruvu Farm. Pia
aliwaomba watanzania kutilia mkazo na kuwekeza katika kilimo hiki kwa
kusema kuwa kilimo ni uti wa Mgongo wa mtanzania na kubainisha kuwa si
lazima mtu kuwa na eneo la hekari kubwa ndio afanye kilimo hiki, La
hasha! bali hata eneo dogo lililoko katika nyumba yako unaweza kutumia
kwa kilimo hiki bila bugudha na kupata mavuno mazuri na pesa nyingi bila
kuhangaika kuwaza kupata eneo la shamba. “Baadhi ya Watu wanadhani na
kuogopa kuwa wataingia gharama kununua eneo la shamba hekari nzima
kwaajili ya kilimo hiki, sivyo kabisa ukiwa na kaeneo kako kadogo katika
nyumba yako na unalima na kuvuna unapata pesa bila taabu yoyote,
tugutuke watanzania maana kilimo ndicho uti wa mgongo kwani nchi
nyingine kama Kenya wamewekeza zaidi katika kilimo hiki” aliongeza.
Hata hivyo pamoja na kumpata mtaalamu huyu wa kilimo hiki Njia mpya bado tunahitaji wataalamu wengi zaidi
ili kufikia kila kona ya Tanzania ili kuweza kuwahudumia wakulima wote
kwa karibu kutokana na hitaji kubwa la wataalamu wanaohitajika. Kama
wewe au rafiki yako ni Mtaalamu au Mshauri wa kilimo hiki Tafadhali
wasiliana nasi kupitia namba zetu au tovuti yetu hapo chini.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Fahamu mbinu za kuongeza thamani nyama
Safari ya kuongeza thamani nyama ya mifugo huanzia shambani kwa usimamizi wa ufugaji na uzalishaji. Lishe bora ni muhimu kwa wa ufugaji ...

-
Mpenzi msomaji wa blog hii leo napenda nikuletee kitu kingine tofauti kidogo na ambacho blog nyingi za kilimo, ntapenda kukuletea...
-
KILIMO BORA CHA KUNDE KILIMO BORA CHA KUNDE : Kunde ni zao ambalo linaweza kulimwa kwa ajili ya chakula na biashara, pia ni zao le...
No comments:
Post a Comment