NAMNA YA KUTUNZA KUMBUKUMBU KATIKA UFUGAJI WA KUKU
NAMNA YA KUTUNZA KUMBUKUMBU KATIKA UFUGAJI WA KUKU
NAMNA YA KUTUNZA KUMBUKUMBU KATIKA UFUGAJI WA KUKU : Kwa mfugaji
yeyeote yule wa kuku ni lazima aweze kujijengea utaratibu wa kuandika na
kutunza kumbukumbu wa kuku wake. Usipo kuwa na utaraitibu huo, jiandae
kusikia ule usemi usemao.”mali bila daftari hupotea bila habari“. Hivyo ni vyema ukiwa na mradi wowote wa ufugaji ni vema ukiwa unaweka kumbukumbu za kila siku au kwa kila wiki.
KATIKA KUTUNZA KUMBUKUMBU ZA UFUGAJI KUNA MAMBO MUHIMU YA KUYAZINGATIA KAMA IFUATAVYO:-
Kumbukumbu za kuku na uzalishaji
Hii ni kuanzia unapowapokea hadi kuwatoa bandani. Hapa unapaswa kila
siku uwaangalie kuku wako ili kujua wanahali gani na ni wangapi waliopo,
hapo utaelewa kama kuna ugonjwa wa kutibu au tahadhari gani
zichukuliwe.
kama ni kuku wa mayai basi kujua idadi ya mayai wanyotaga kila siku,
ili uweze kujua asilimia za utagaji na uweze kupima kiwango chao cha
utagaji.
Kumbukumbu za chanjo.
Weka kumbukumbu za chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali kama vile mdondo (Newcastle), gumboro, ndui na magonjwa mengine.
Kumbukumbu za afya.
Hapa unarekodi kila aina ya ugonjwa uliotekea bandani, idadi ya
walioathirika, waliotibiwa, waliopona na waliokufa. Gharama za matibabu
nazo pia ziwekwe kwenye kumbukumbu.
Gharama za vifaa na chakula.
Vifaa vyote unavyonunua kwa ajili ya ufugaji ni lazima viorodheshwe
na viwekwe kwenye kumbukumbu, na gharama za chakula kuanzia unapoingiza
kuku hadi unapowatoa iwekwe kwenye kumbukumbu pia.
MUHIMU: Njia rahisi ya kutunza kumbukumbu ni kununua daftari na kutengeneza majedwali yanayoonesha vipengele tajwa hapo juu
No comments:
Post a Comment