Wednesday, July 17, 2024

Fahamu mbinu za kuongeza thamani nyama

 

Safari ya kuongeza thamani nyama ya mifugo huanzia shambani kwa usimamizi wa ufugaji na uzalishaji. Lishe bora ni muhimu kwa wa ufugaji wa mifugo wa nyama, hivyo, nyama nzuri huanza na lishe bora. Malisho ya hali ya juu yasiyokuwa na vimelea vinavyoweza kusababisha magonjwa na kemikali hatari yanakidhi mahitaji ya lishe ya mnyama. Hii itahakikisha mnyama anapochinjwa anatoa nyama laini isiyokuwa na mafuta mingi. Na hii hupendwa na walaji wengi.

Ukaushaji wa nyama

Nyama inauzwa nchini kwa njia mbalimbali na kwa urahisi ili kukidhi mahitaji ya walaji. Nyama huwa na thamani kubwa ya kibayolojia na huchangia katika kupambana na utapiamlo na upungufu wa protini ambayo ni shida kuu mbili katika nchi nyingi za Afrika, ikiwemo Tanzania.

Kutokana na hilo, msisitizo mkubwa unawekwa katika kuimarisha teknolojia zinazofaa za kutengeneza bidhaa za nyama ili kukidhi hali ya watu, hasa walio maeneo ya vijijini.

Matumizi ya nyama katika utengenezaji wa bidhaa inasisitizwa kwa sababu yana ubora wa virutubishi kama vile protini ya hali ya juu, vitamini, madini mengine vya umuhimu mkubwa kwa mwili wa binadamu.

Kuhifadhi nyama

Kukausha nyama kutumia joto la asili, unyevu na mzunguko wa hewa, ikiwa ni pamoja na miale ya jua ya moja kwa moja ni njia ya tangu jadi ya kuhifadhi nyama. Inajumuisha kupunguza maji iliomo kwenye vipande vya nyama vilivyokatwa-katwa ili kuruhusu kukauka kwa utaratibu.

  • Nyama isiyokuwa na mafuta inafaa kwa kukausha na ikiwezekana iwe nyama ya mnyama wa umri wa kati na aliye katika hali nzuri.
  • Kata nyama katika vipande virefu vinavyofanana na inayofuata nyuzi za misuli. Urefu wa vipande unaweza kutofautiana, ingawa haipaswi kuwa chini ya sentimita 20 na isizidi senstimita 70. Nyama iliyokatwa vipande vifupi inahitaji muda mwingi zaidi kuyaweka pamoja kuliko ile iliyokatwa vipande virefu. Lakini, vipande ambavyo ni virefu sana vinaweza kuvunjika kwa sababu ya uzito wake.
  • Unene wa vipande huamua muda wa mchakato wa kukausha. Kwa kuwa vipande vinene huchukua muda zaidi kukauka kuliko vile vyembamba, ni muhimu kwamba vipande vya kuwekwa kwenye kundi moja ziwe zinafana kwa urefu na unene.
  • Weka vipande ndani ya maji ya chumvi kwa muda wa dakika 5 (ndani ya saa 5 baada ya kuchinja) kisha ondoa maji kwa kutumia chujio. Chumvi huzuia ukuaji wa vijidudu na kuwazuia nzi.
  • Tumia waya ya chuma usioshika kutu kuzishikilia vipande vya nyama. Simamisha au ning’iniza kila kipande cha nyama kutoka mwisho ili kuhakikisha mzunguko wa hewa na kukausha kwa haraka. Epuka vipande vya nyama kugusana kwa kuwa maeneo yaliyogusana yatabaki na unyevu kwa muda mrefu, na kuleta mazingira mazuri ya uharibifu, bakteria na inzi. Vipande vya nyama vilivyofungwa kwenye waya wa chuma vinaweza kusimamishwa kwenye mbao, Kamba au waya.
  • Ning’iniza kwenye nguzo iliyotengenezwa kwa mbao au chuma. Kausha kwa muda wa siku 4 hadi 5 na baada ya kipindi hiki, nyama iko tayari kwa matumizi, ufungashaji au usafirishaji.
  • Wakati wa ukavu, nyama iliyokatwa vipande vyenye umbo hizi mbili ndio hufaa zaidi kwa ukaushaji wa asili: vipande viliyokatwa mstatili wa sentimita 1 x 1 na vipande vilivyokatwa umbo la jani wa sentimita 0.5 x takribani sentimita 3, 4 au 5.

Viwango vya ubora wa nyama iliyokaushwa

Kukausha nyama inachukua siku nne hadi tano. Baada ya kipindi hiki nyama iliyokaushwa iko tayari kwa matumizi na inaweza kufungwa, kuhifadhiwa au kusafirishwa. Ni vyema kuhakikisha kwamba bidhaa hii inafikia vigezo vifuatavyo vya ubora.

  • Muonekano wa nyama kavu lazima iwe ya usawa iwezekanavyo. Uwepo wa mikunjo ni ishara kwamba nyama imekauka vizuri. Rangi yake isiwe nyekundu ya damu bali nyekundu yenye weusi kidogo.
  • Nyama iliyokaushwa inapaswa kuwa na ladha ya chumvi kidogo, hasa kama imekaushwa asili bila viungo. Harufu mbaya haipaswi kutokea. Nyama iliyokaushwa iliyo na mafuta mengi haipaswi kuhifadhiwa kwa muda mrefu, lakini itumike haraka iwezekanavyo ili isiharibike.
  • Nyama iliyokaushwa lazima ichunguzwe mara kwa mara ili kubaini harufu inayohusiana na kuharibika, ambayo ni matokeo ya utayarishaji usio sahihi au ukaushaji wa nyama. Nyama iliyo na dalili za kuharibika lazima ichaguliwe na kutupwa.
Beef Jerky

Soseji

Soseji ni aina ya bidhaa ya nyama ambayo kwa kawaida hutengenezwa kutokana na nyama ya kusagwa mara nyingi nyama ya nguruwe, nyama ya ng’ombe, au kuku, pamoja na chumvi, viungo na ladha nyinginezo.

Viungo vingine, kama vile nafaka au mkate vinaweza kujumuishwa kama vichungi au virefusho.

Wednesday, July 10, 2024

KILIMO BORA CHA BAMIA

 KILIMO BORA CHA BAMIA
Bamia ni zao la mbogamboga linalotambulika kitaalamu kama Abelmoschus esculentus lenye
asili ya Ethipia na Afrika ya magharibi. Kwa sasa zao hili linalimwa katika nchi nyingi hasa
sehemu za joto. Baadhi ya maeneo yanayolima zao la bamia kwa Tanzania ni pamoja na mikoa
ya Morogoro, Dodoma, Tabora, Pwani na Mbeya.
MATUMIZI YA BAMIA
Zao hili hulimwa kwa ajili ya matunda yake ambayo hutumika kama mboga au kiungo katika
mapishi mbalimbali majumbani. Vilevile katika nchi zilizoendelea nyuzi nyuzi zinazotokana na
zao hili hutumika katika utengenezaji wa karatasi.
AINA ZA MBEGU
Kuna aina tofauti za mbegu za bamia zinazo patikana Tanzania kama vile Clemson Spineless,
Emerald Green, White Velvet, Perkins Mammoth na Dwarf Prolific. Mbegu ambazo hutumika
na wengi ni
Clemson spineless. Mbegu hii inatabia ya kukua urefu wa mita 1 hadi 1.5 na kuzaa bamia za
kijani zenye urefu karibu sm 15. Huchukua siku 55 hadi 58 kuanza kuvuna.
Emerald green. Mbegu hii ina tabia ya kukua hadi urefu wa m 1.5 na kuzaa bamia za kijani
zenye urefu wa sm 18 hadi 20. Huchukua siku 58 hadi 60 kuanza kuvuna.
White velvet. Mbegu hii inatabia ya kukua urefu wa m 1.5 hadi 1.8 na kuzaa bamia ndefu,
nyembamba, zilizochongoka na zenye urefu wa sm 15 hadi 18.
Bamia aina ya Emerald green
UCHAGUZI WA ENEO
Ni muhimu kuchagua eneo linalofaa kwa kilimo cha bamia kabla ya kuanza uzalishaji. Ni vyema
eneo litakalotumika katika kilimo cha bamia liwe na urahisi wa upatikanaji maji kurahisisha
umwagiliaji kwa kilimo cha umwagiliaji. Vilevile shamba liwe lenye kufikika kwa urahisi ili
kufanya wepesi katika kuhudumia shamba na usafirishaji wa mazao kwenda sokoni au kufikiwa
kwa urahisi na wanunuzi wanaofuata mazao shambani.
Zao la bamia hushambuliwa sana na minyoo fundo (nematodes). Hivyo usichague eneo ambalo
limetoka kutumika katika kilimo cha mazao yanayoweza kushambuliwa na minyoo fundo kama
vile viazi vitamu, nyanya, bilinganya na pilipili hoho. Kwa tahadhari unaweza kulima zao hili
katika eneo ambalo limetoka kutumika kwa kilimo cha mazao ya nafaka kama vile mahindi na
mtama kwa kuwa mazao haya hayashambuliwi na minyoo fundo.
MAHITAJI YA KIIKOLOJIA
HALI YA HEWA NA MWINUKO
Bamia ni zao linalopendelea hali ya joto hivyo hustawi katika maeneo yenye hali joto kuanzia
nyuzi joto za sentigredi 21 hadi 35. Ustawi mzuri zaidi huonekana katika maeneo yenye joto la
nyuzi za sentigredi 21 mpaka 30. Hali joto zaidi ya nyuzi za sentigredi 42 huweza kusababisha
kudondoka kwa maua. Bamia hustawi vizuri katika maeneo ya mwinuko tofauti hadi mita 1000
kutoka usawa wa bahari yenye mvua za wastani.
UDONGO
Zao la bamia hustawi katika udongo wa aina nyingi wenye rutuba, kina, uwezo wa kuifadhi maji
vizuri na usiotuamisha maji. Hata hivyo zao hili hufanya vizuri zaidi linapolimwa katika udongo
wa tifutifu yenye kichanga wenye rutuba ya kutosha na tindikali kuanzia Ph 5.8 hadi 6.5. Mbegu
za bamia hushindwa kuota kabisa pale joto la udongo linapokuwa chini ya nyuzi za sentigredi
16.
KUANDAA SHAMBA
MUDA WA KUANDAA
Shamba la bamia liandaliwe mapema mwezi mmoja kabla ya kupanda ili kuruhusu magugu na
mabaki ya mazao kuoza vizuri. Kwa kilimo cha kutegemea mvua ni vyema maandalizi yaanze
mapema kabla ya kuanza kwa mvua za masika. Inashauriwa kuanza maandalizi mapema mwezi
Januari. Kwa kilimo cha umwagiliaji unaweza kuanza maandalizi muda wowote kulingana na
mahitaji na soko unalolilenga.
NAMNA YA KUANDAA
Shamba huandaliwa kwa kufyeka nyasi, kung’oa visiki na kulima kabla ya kupima na kuweka
matuta.
(i) KULIMA
Shamba hulimwa kwa kutumia jembe la mkono, jembe la kukokotwa na wanyama, power
tillers au matrekta. Matumizi ya jembe la kukokotwa na wanyama, power tillers na matrekta
hurahisisha shughuli ya kulima na kuifanya iwe na ufanisi kwani hukatua udongo vizuri na
kuufanya uwe tifutifu. Unapotumia jembe la mkono katika kulima hakikisha unakatua udongo
katika kina cha kutosha sm 20 mpaka sm 30 na kulainisha mabonge. Udongo uliokatuliwa vizuri
hupitisha hewa inayohitajika na mmea, hurahisisha ukuaji wa mizizi na kuifadhi maji vizuri.
(ii) KUPIMA SHAMBA (FIELD LAYOUT)
Ni muhimu kuanza kupima shamba kabla ya kuanza kuandaa matuta ili kupata matuta yaliyo
katika mpangilio mzuri na mistari ya mimea shambani iliyonyooka vizuri. Kabla ya kupima
matuta ni muhimu pia kujua nafasi ya kupandia utakayo tumia ili kupata ukubwa sahihi wa kila
tuta.
Kwa mfano kwa nafasi ya kupandia ya sm 60 × sm 40 kwa matuta makubwa unaweza
kutengeneza kila tuta katika upana wa sm 1.2 na urefu wowote. Acha nafasi ya m 1 kuzunguka
shamba na njia kila baada ya tuta upana wa sm 50. Tumia Tape measure au kamba yenye vipimo
kupima shamba huku ukiweka alama za matuta na njia kwa kuchomeka mambo (pegs) katika
kila kona ya tuta na kuzungushia kamba.
(iii) KUWEKA MATUTA
Inashauriwa kupanda bamia katika matuta ili kusaidia mizizi kukua vizuri na udongo kuhifadhi
maji. Wakati wa kiangazi, tengeneza matuta yaliyodidimia kidogo ili kufanya maji yaweze kukaa
kwenye udongo na wakati wa masika matuta yainuliwe kidogo toka kwenye usawa wa ardhi ili
kuzuia maji yasituame. Matuta yanaweza kuwa makubwa au madogo kulingana na matakwa ya
mkulima. Matuta makubwa hupandwa mistari miwili na matuta madogo hupandwa mstari
mmoja. Tengeneza matuta kwa kufuata alama zilizowekwa wakati wa kupima shamba.
UPANDAJI WA BAMIA
Zao la bamia huweza kupandwa moja kwa moja shambani au kwa kuanzia kitaluni. Hata hivyo
wakulima wengi hupendelea zaidi kupanda zao hili moja kwa moja shambani pasipo kupitia
kitaluni. Katika eneo lenye udongo mzito wenye asili ya mfinyanzi mbegu hupata shida kuota
hivyo ni muhimu kuanzia kitaluni ili kuweza kupata miche mingi shambani. Kwa kuanzia
kitaluni hakikisha unafuata taratibu zote za uandaaji na matunzo ya kitalu cha mbogamboga na
pandikiza miche pindi inapokua na majani halisi matatu hadi manne.
MAANDALIZI YA MBEGU
Mbegu za bamia ni ngumu kidogo katika kuota hivyo ni vyema ziandaliwe ili kurahisisha uotaji
wake. Mbegu za bamia huandaliwa kwa kuziloweka katika maji ya vuguvugu kwa muda wa
masaa ishirini na nne ili kuchochea uotaji. Mbegu za bamia huchukua muda wa siku 5 hadi 10
kuota. Kutegemeana na nafasi ya kupandia na uotaji wa mbegu kiasi cha kilo moja na nusu hadi
kilo mbili na nusu za mbegu kinaweza kutosha kupanda katika eneo la ekari moja.
Bamia aina ya clemson spineless
NAFASI YA KUPANDIA
Bamia huweza kupandwa katika nafasi tofauti kuanzia sm 60 hadi 80 kati ya mstari na mstari na
sm 30 hadi 50 kutoka shimo hadi shimo.Hakikisha unafuata maelekezo ya mbegu husika juu ya
nafasi pendekezwa.
HATUA ZA UPANDAJI
Unaweza kufuata hatua zifuatazo katika upanzi wa mbegu za bamia shambani:
1 – Mwagia maji mengi shambani masaa kumi na mbili kabla ya kupanda mbegu ili kulainisha
udongo na kurahisisha upanzi.
2 – Chimba mashimo ya kupandia yenye kina cha sm 2 hadi 3 katika nafasi iliyopendekezwa
kwa mbegu itakayotumika mistari miwili miwili kila tuta kwa kutumia kamba iliyowekwa
vipimo.
3 – Weka viganja viwili vya mkono vya samadi iliyoiva katika shimo la kupandia kisha
changanya na udongo kupata mchanganyiko mzuri. Kwa mbolea ya kupandia kama DAP weka
nusu kizibo cha soda katika kila shimo la kupandia kisha fukia mbolea kwa tabaka dogo la
udongo kabla ya kupanda mbegu. Kiasi cha kilo hamsini za mbolea ya DAP kinatosha kutumika
katika eneo la ekari moja.

Fahamu mbinu za kuongeza thamani nyama

  Safari ya kuongeza thamani nyama ya mifugo huanzia shambani kwa usimamizi wa ufugaji na uzalishaji. Lishe bora ni muhimu kwa wa ufugaji ...