JINSI YA KUONGEZA RUTUBA KWENYE SHAMBA LAKO

Ili kuvuna mazao mengi lazma udingo unao lima uwe na rutuba ya kutosha ili kusababisha mazao yako kupata virutubisho muhimu kwa ukuaji

zifuatazo ni njia ambazo zitakusaidia mkulima kuongeza rutuba kwenye shamba lako
  usipande mazao ya aina moja kwa mfululizo, hautakiwi kupanda mazao ya aina moja mfano mahindi na mtama kwa kufuliuliza ili kuepusha virutibisho kupotea vyote  na itasababisha magonjwa na wadudu kuwa wengi shambani

usitumie mbolea za kemikali mara kwa mara,hii pia haitakiwi, mbolea za kemikali mfano UREA hua hazitajkiwi kutumika mara kwa mara husababisha alzi kupunguza rutuba mbolea hizi utumika mara moja moja zinapo itajika.

 usipende sana kuchoma shamba, unapo choma shamba unasababisha kuuwa wadudud wanao sababisha kuongeza rutuba kwenye udongo na pia huua uoto asiri.

 zika mabaki ya mazao baada ya kuvuna, unapo vuna mabaki ya mazao mfano mabua yanapo zikwa na kuoza husababisha kuongeza rutuba kwenye udongo husika.

panda mazao ya jamii ya mikunde, pia mazao ya mikunde mfano kunde na maharage husaidia kuongeza naitrogen ambayo inatakiwa sana na mimea hivo rutuba huongezeka

weka mbolea ya samadi ,hii ni mbolea hasiri inayo yani ni kinyesi cha ng'ombe hivo ili kuongeza rutuba inabidi uweke sana samadi kwenye shamba lako hii itasaidia sana kurudisha rutuba kwenye shamba lako.

pumzisha shamba, Wakulima wengi hua hawapendi kupumzisha shamba hivo wanashauliuwa kupumzisha shamba kwa mda hii usaidia shamba kuongeza rutuba iliyo kua imepotea.

usitumie sana viuagugu,hii pia ni mbaya kutumia ke mikali za viuagugu badala yake palilia kwa jembe na badae yazike magugu ili rutuba iendelee kubaki kwenye shamba lako.

usitifue kupita kipimo, hii husababisha mmomonyoko wa udongo na pia rututba nyingi hupote kwa huo mmomonyoko

Comments

Popular Posts