Saturday, November 25, 2017

Kilimo cha Kisasa: Kilimo bila Jua, Udongo wala Maji Mengi

:
shamba_la_kisasa
Kwa kawaida kilimo kinahitaji maji, urdhi ya kutosha, jua n.k. Lakini hali ni tofauti kwa kampuni ya AeroFarms ambayo imekuja na mawazo tofauti ya kulima mazao mbalimbali bila kutumia udongo, jua wala maji mengi.
Kilimo chao hufanyika ndani ya nyumba tena kwenye ghala la zamani; hii ina maana kuwa kilimo hiki kinaweza kufanyika popote bila kuathiriwa na hali ya hewa.
Wazo hili lilianzishwa na Ed Harwood, ambaye ni profesa kwenye Chuo cha kilimo cha Cornel aliyetaka kupanda vitu bila kutumia vitu vinavyokuza vitu.

Kilimo bila ardhi au udongo

AeroFarms wametengeneza vitu kama rafu au shelfu ambavo zina vitambaa maalumu ambavyo mbegu husiwia juu yake badala ya udongo. Mizizi ya mmea husika hujishikiza katika kitambaa hicho kuelekea chini kujipatia virutubisho na maji.

Rafu/Mashelfu ya aeroponic

Kilimo bila maji mengi

AeroFarms hawatumii maji mengi kama ilivyo kwa kilimo cha kawaida ambacho hutumia zaidi asilimia 70 ya maji; kwani wao hutumia ukungu wenye virutubisho vinavyohitajika na mmea. Teknolojia hii inajulikana kama kupanda mimea bila udongo wala maji mengi “aeroponics”; hii ina maana kuwa mimea hii hutumia maji kidogo kuliko ile ya kilimo cha kawaida.
shamba lote
Mchoro wa teknolojia ya aeroponic.

Kilimo bila jua

Katika kilimo hiki AeroFarms hawatumii jua kukuza mimea yao bali hutumia taa maalumu za LED ambazo pia zinaokoa nishati. Kwa njia hii wanaweza kutawala kiasi cha mwanga, rangi ya mazao, virutubisho, na hata ladha na ubora wake.

Je kilimo hiki kina tija?

Kwa mujibu wa AeroFarms wanadai kuwa mavuo katika kilimo hiki ni mara 130 zaidi kwa mita za mraba ukilinganisha na shamba la kawaida. Pia wanadai hutumia asilimia 95 pungufu ya maji na asilimia 40 pungufu ya madawa ukilinganisha na kilimo cha kawaida. Taarifa zinaonesha kuwa AeroFarms wameshapata faida zaidi ya dola milioni 100 hadi sasa.
bidhaa_za_aer
Bidhaa zilizokamilika
Je una maoni gani kuhusu kilimo hiki? Je kinafaa kwa mazingira yetu ili tutunze mazingira? Tuuandikie maoni yako kisha washirikishe wengine.
  • Makala za Mwandishi

Kilimo cha Kisasa cha Mahindi



Kulingana na msimu mahindi hupandwa mwanzoni mwa mwezi wa 11 baada ya mvua za kwanza kunyesha (specifically from 1st to 15th day of November) ambayo huvunwa mwezi Machi mwishoni au aprili mwanzoni. Pia mahindi hupandwa mwanzoni mwa mvua za masika yaani mwezi wa pili mwishoni na mwezi wa tatu mwanzoni ambayo huvunwa mwezi Julai katikati na Agosti mwanzoni....


KUANDAA SHAMBA, KUPANDA NA KUPALILIA


Kuandaa Shamba, Kusafisha, Kulima/Kutifua
Ni vyema mashamba yaandaliwe mapema kabla ya msimu wa kupanda haujaanza ili kumpa mkulima fursa ya kupanda kwa wakati unaotakiwa. Kuna njia mbalimbali zinazotumika kuandaa mashamba. Kati ya njia hizi ni pamoja na kufyeka, kung’oa visiki na kulima. Shamba linaweza kulimwa kwa kutumia:
  • Jembe la mkono - wengi wanatumia
  • Jembe la kukokotwa na wanyama kama ng’ombe
  • Power tillers
  • Matrekta
Matumizi ya trekta, power tillers na jembe la kukokotwa na wanyama yanapunguza nguvu kazi kwani vinachimbua udongo na kuufanya kuwa tifutifu (kufanya isiwe na mabonge makubwa, wala isiwe vumbi vumbi). Hii husaidia:
  • Mizizi ya mimea kupenyeza ardhini kirahisi
  • Udongo kuweza kuhifadhi maji
  • Udongo kuwa na hewa inayohitajika na mimea
  • Ukuaji mzuri wa mimea hivyo kuongeza mavuno
Mbegu Bora za mahindi
Matumizi ya mbegu bora ni muhimu katika upatikanaji wa mavuno mengi na bora. Kuna makundi mawili makuu ya mbegu ambayo ni:
  • Mbegu za asili: Ni zile ambazo zimetumika miaka mingi katika historia ya kilimo
  • Mbegu zilizoboreshwa: Hizi ni zile zilizoboreshwa kutoka mbegu za asili. Kundi hili linagawanywa kwenye makundi mawili - composite varieties na mbegu chotara (Hybrids).
Ushauri wa matumizi ya mbegu zilizoboreshwa unatofautiana kutoka eneo moja na lingine kwa sababu ya:
  • Mwinuko kutoka usawa wa bahari
  • Kiasi cha mvua katika eneo husika
  • Muda unaotumia mbegu hadi kukomaa
Mbegu za mahindi zilizoboreshwa ni kama TMV1, TAN 250, TAN 254, Staha, Situka na zingine zote zinazoanza na herufi “H” kama vile H 250, H 251 na H 615. Pia mbegu mpya zilizotangawa na Kamati ya Taifa ya Mbegu mwaka huu ni WE4102, WE4106, WE4110, WE4114, WE4115 kutoka ARI ILONGA.

Jinsi Ya Kuweka Mbolea Za Kupandia
Mbolea hizi zinawekwa shambani kabla ya kupanda/kusia mbegu. Zinawekwa kwa njia mbalimbali kama vile kusambaza kwenye eneo husika na kuchanganya na udongo, au kuweka kwenye mistari au mashimo ya kupandia. Ni bora zaidi kuchanganya mbolea za Minjigu Phosphate au Minjingu Mazao na udongo kuliko kutia kwenye shimo la kupandia. Pia kuchanganya mbolea na udongo huondoa athari za mbolea kwenye uotaji wa mbegu, hasa kama kuna uhaba wa unyevunyevu.
Viwango Vya Mbolea Za Kupandia mahindi
Kiwango cha mbolea za kupandia kilichopendekezwa ni kilo 20 fosfati (P) kwa hektari ambayo ni sawasawa na kiasi cha mifuko 2 ya DAP (= mfuko mmoja kwa ekari). Ikiwa mbolea ya minjingu phosphate itatumika basi mifuko mitatu itatosa kwa hekta (= mfuko mmoja na nusu kwa ekari). Na endapo utaamua kuitumia mbolea ya minjingu mazao basi tumia mifuko minne na nusu kwenye hekta moja au mifuko miwili kwa ekari moja.
 


Upandaji wa mahindi
Muda wa kupanda: Kulingana na msimu mahindi hupandwa mwanzonimwa mwezi wa 11 baada ya mvua za kwanza kunyesha (specifically from 1st to 15th day of November) ambayo huvunwa mwezi Machi mwishoni au aprili mwanzoni. Pia mahindi hupandwa mwanzoni mwa mvua za masika yaani mwezi wa pili mwishoni na mwezi wa tatu mwanzoni ambayo huvunwa mwezi Julai katikati na Agosti mwanzoni. Katika msimu huu utayarishaji wa shamba hufanyika mwezi wa pili mwanzoni.
Muda wa kupanda unatofautiana kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na majira ya mvua. Kwa mfano katika wilaya ya Morogoro tarehe za kupanda ni kuanzia februari 15 hadi Machi 15. Mkulima anashauriwa afuate kalenda ya muda wa kupanda kama anavyoshauriwa na bwana shamba wake.
Nafasi ya kupandia mahindi
Kupanda kwa nafasi ni kati ya njia bora za kilimo inayomwezesha mkulima kupata mazao bora. Hivyo ni muhimu sana kuzingatia kupanda kwa mistari na kufuata nafasi zinazoshauriwa na wataalamu wa kilimo. Zifuatazo ni nafasi za kupanda mahindi na idadi ya mbegu kwa kila shimo na kiasi cha mbolea (kwa vizibo vya soda) inayotakiwa kuwekwa kwa shimo:
  • Kwa nafasi ya 90 sm X 30 sm, panda mbegu moja na uweke kizibo kimoja cha mbolea
  • Kwa nafasi ya 90 sm X 25 sm, panda mbegu moja na uweke kizibo kimoja cha mbolea
  • Kwa nafasi ya 90 sm X 50 sm, panda mbegu mbili na uweke vizibo viwili vya mbolea
Kupalilia
Ni muhimu shamba lipaliliwe baada ya mimea kuota ili kuondoa magugu. Magugu ni mimea hivyo hushindana na mimea iliyopandwa na mkulima kwa kunyonya virutubisho ardhini. Magugu yanaweza pia kuhifadhi wadudu na magonjwa yanayoweza kushambulia mimea iliyopandwa na hivyo kupunguza mavuno. Magugu yaweza kuondolewa wa palizi ya mkono (yaani) kung’olea (ikiwa magugu yapo mbali mbali sana) au kulima kwa jembe la mkono au kwa kutumia dawa/viuagugu (HERBCIDES) hasa 2-4D.
Mbolea za kukuzia mahindi
Ni mbolea zinazotumika baada ya mimea kuota kwa lengo la kuikuza mimea ili itoe mavuno bora. Mara nyingi mbolea hizi zinatoa kirutubisho cha naitrojeni. zifuatazo ni mbolea za kukuzia na kiwango chake cha naitrojeni:
  • UREA: 46% N
  • Calcium Ammonium Nitrate, CAN: 23% N
  • Sulphate of Ammonia, SA: 21%
Urea inakirutubisho cha naitrojeni (N) kwa kiwango kikubwa na watu wengi wanauzoefu nayo. Vilevile bei yake ni nafuu ikilinganishwa na mbolea zingine za kukuzia. Mbolea hii iko katika hali ya chengachenga za mviringo (granules) za rangi nyeupe. Kiwango cha urea ni nusu kizibo cha soda kwa kila shina. Mbolea hizi hazidumu kwenye udongo kwa muda mrefu kwa hiyo huwekwa shambani wakati mimea inapokuwa na mahitaji makubwa ya kirutubisho cha naitrojeni na wakati udongo una unyevunyevu na shamba halina magugu.
Pia wakulima hutumia mbolea za kukuzia zinazopatikana kwa bei nafuu kama vile BOOSTER (foliage nitrogeneous fertilizers) ambayo hupigwa kwa kunyunyizia katika majani ya mmea kila baada ya wiki 3, kwa mara 2-3 mpaka mahindi kuvunwa. Kiwango cha kupiga ni mchanganyo wa mls 50-80 ktk lita 15 za maji. Mbolea za kukuzia huwekwa kuzunguka kila shina la mimea au pande mbili au tatu au nne za kila shina. Cha muhimu ni kwamba mbolea isirundikwe sehemu mmoja. Minjingu Mazao (kg 50/ekari = gramu 10kwa shimo) pia yaweza tumika kwa kukuzia, hivyo mkulima yko huru kuchagua kulingana na uwezo na upatikanaji wake.
Viwango Vya Mbolea Za Kukuzia Vinavyoshauriwa
Kiwango kinachopendekezwa ni kilo 60 naitrogeni kwa hektari, ambacho ni sawasawa na kiasi cha mifuko miwili ikiwa utatumia UREA. Hata hivyo mbolea zingine kama SA inaweza kutumika kama kuna mahitaji ya salfa. Hivyo basi utumie mifuko mitatu kwa hekta ambayo ni sawa na mfuko mmoja kwa ekari. CAN inaweza kutumika kama kuna mahitaji maalum ya nitrate na ammonium na endapo utaitumia basi mifuko minne na nusu itatosha kwa hekta, ambapo kwa ekari moja utatumia mifuko miwili tu. 
Kwenye mahindi mbolea ya kukuzia inawekwa baada ya palizi ya kwanza ambayo ni kama wiki tatu mpaka wiki nne baada ya kupanda. Kwa kila mmea mmoja weka kiasi hiki cha mbolea:
  • UREA: kizibo kimoja cha soda
  • CAN: vizibo viwili vya soda, na 
  • SA: kizibo kimoja cha soda
Mambo Muhimu Ya Kuzingatia
Kuweka mbolea: Sehemu za nchi ambazo muda wa kukua mahindi ni mrefu (zaidi ya miezi mitatu), ni vyema kuweka mbolea za kukuzia mara mbili, yaani nusu ya kiwango kinachopendekezwa baada ya mwezi mmoja, na kurudia tena (kutumia nusu iliyosalia) baada ya wiki tatu.
Kupalilia: Katika kilimo cha mahindi, ni muhimu shamba lipaliliwe siku 14 hadi 21 baada ya mimea kuota kufuatana na hali ya shamba wakati wa kupanda. Wataalamu wanashauri kwamba katika kilimo cha mahindi, shamba lipaliliwe mara 2-3, kufuatana na hali ya magugu katika shamba.
- Utafiti unaonyesha kwamba, shamba la mahindi ambalo halijapaliliwa linaweza kupunguza mavuno kwa asilimia 60 hadi 100 ya mavuno yanayotarajiwa. Hata kama mkulima atatumia mbegu bora, aina na kiasi cha mbolea zinazoshauriwa, kupanda kwa mstari pamoja na mbinu nyingine bora zinazoshauriwa, bila kupalilia hali hii itaathiri mavuno yake.

KUDHIBITI MAGONJWA NA WADUDU WANAOSHAMBULIA MAHINDI

Magonjwa Yanayoshambulia Mahindi

i) Maize streak virus
Dawa/Kudhibiti: Mbegu bora inayostahimili ugonjwa, kupanda mapema, kung’oa mimea iliyoathirika ama kunyunyiza dawa za kuua ‘vectors’ kama vile inzi weupe (white flies).
ugonjwa-wa-maize-streak-virus
Maize streak virus
ii) Smut (Fugwe)
Dawa/Kudhibiti: Tumia Helerat ukifuata maagizo kamili.
ugonjwa-wa-smut-wa-mahindi
Ugonjwa wa fungwe kwenye mahindi
iii) Cob rot (kuoza kwa mhindi)
Dawa/Kudhibiti: Tumia mbegu zinazostahimili kuoza.
Ugonjwa-wa-kuoza-muhindi
Muhindi uliooza

Wadudu Na Wanyama Wanaoshambulia Mahindi

a) Viwavi Jeshi
Ni wadudu aina ya funza ambao hutokana na Nondo.Hushambulia mahindi kwa kula majaniyake pamoja na shina. Wadudu hawa huangamizwa/kudhibitiwa kwa njia zifuatazo;-
  • Kuondoa vichaka karibu na shamba
  • Kunyunyizia sumu za asili kama vile Mwarobaini majuma mawili ya mwanzo.
  • Kunyunyizia sumu za viwandani endapo wadudu wameanza kuonekana kama vile Karate 1ml/1L
viwavi-jeshi
Viwavi jeshi
b) Funza wa Mabua (Maize Stalk Borer)
Funza wa mabua hutoboa shina la mahindi na kusababisha kudumaa kwa mahindi.
  • Matundu, ungaunga kama wa msumeno huonekana kwenye majani yaliyoathiriwa.
  • Mashambulizi huanza juma la pili hadi la tatu baada ya mahindi kuota.
  • Njia za kudhibiti zinazotumika
  • Kuchanganya mahindi na mazao jamii ya mikunde km vile maharagwe
  • Kung’oa mahindi yaliyoshambuliwa
  • Sumu za asili mwarobaini
  • Sumu za viwandani km vile Karate. pia waweza tumia Malathion, sumithion, vumbi ya cymbush au Sevin 5G na ufuate maagizo kamili.
funza-wa-mahindi
Funza wa mabua

c) Cutworms (Vikata Shina)
Dawa/Kudhibiti: Tumia Dragnet FT na ufuate maagizo kamili.

d) Wanyama waharibifu
Kudhibiti: Kuwatishia na kuwafukuza wanyama.
Ili mkulima aweze kupata mazao mengi na bora inashauriwa kutumia dawa za kuzuia magonjwa na wadudu washambuliao mimea na njia zinginezo.



Nyani
Nyani

KUVUNA, KUKAUSHA, KUSAFISHA NA KUHIFADIHI

Kuvuna
Mahindi yako tayari kuvuna wakati kikonyo kimekuwa dhaifu na mahindi yanaangalia chini. Mahindi yakishakauka vizuri yanatenganishwa na bua halafu majani ya mhindi kutolewa.
Kukausha
Kama mahindi hayajakauka vizuri hukaushwa zaidi katika juani siku 3-4 ili kupunguza unyevunyevu kufikia kiwango kinachofaa kwa kuhifadhi (14%). Ni muhimu mahindi yakauke vizuri ili yasioze yakiwekwa ghalani. Ili kujua kama mahindi yamekauka vizuri, tia mahindi kadhaa kwenye chupa ya soda iliyokauka na uongeze kiganja kimoja cha chumvi. Tingisha chupa halafu uwache itulie kwa dakika tatu. Chumvi ikikwama kando ya chupa, basi mahindi hayajakauka vizuri.


Kusafisha
Mahindi yaliyokauka vizuri hupepetwa na vilevile mahindi mabovu huondolewa.
Kuhifadhi
Mahindi huhifadhiwa ghalani baada ya kuwekwa viatilifu vya kuzuia bungua wa mahindi Njia za kisasa za uhifadhi hutumiwa kama vile matumiz ya ACTELLIC SUPER DUST katika uwiano wa 1kg kwa gunia 5-10 za ujazo wa 100kg. Kiatilifu kingine ni actellic solution katika rate ya 5mls katika gunia moja la kg 100. Njia nyingine ya kienyeji katika kuhifadhi mahindi ni kuweka juu ya ghala ambalo chini yake kuna jiko la kupikia ambalo hutoa moshi unaotumika kufukuza na kuua wadudu.

Pia waweza kufahamu:
Tafadhali weka comment yako hapa chini ili kubadilishana uzoefu na wakulima wengine.

Friday, November 3, 2017

CHAKULA CHA NGURUWE NA ULISHAJI


A.    Utangulizi

Chakula bora kwa Nguruwe ni moja  ya suala muhimu sana kwenye dhana nzima ya ufugaji wa Nguruwe wenye tija na faida kwa mfugaji. Chakula cha Nguruwe kinagharimu kama asilimia sabini ya garama zote za ufugaji wa nguruwe. Kati ya matatizo mengi yanayosababisha tija na ufanisi duni wa uzalishaji wa Nguruwe yanatokana na lishe duni. Lakini kama wakipatiwa lishe bora, tija na ufanisi wa uzalishaji utakuwa mkubwa hivyo kuongeza faida kwa mfugaji.

B.       Baadhi ya faida za kulisha lishe bora kwa nguruwe

1.     Lishe bora huharakisha ukuaji wa haraka wa Nguruwe nahivyo kupata uzito unaohitajika kwa kipindi kifupi.
2.    Lishe bora hupunguza gharama za ufugaji na hivyo kuongeza faida kwa mfugaji kwa sababu nguruwe atahitaji kiasi kidogo tu cha chakula na atachukua muda mfupi kupata uzito mkubwa
3.  Lishe bora itapunguza maambukizi ya magonjwa.
4.  Lishe bora huongeza kiasi cha mayai yatakayoivishwa na mama Nguruwe na hivyo kuongeza idadi ya watoto watakaozaliwa

5.    Lishe bora huongeza kiasi cha maziwa yatakayotengenezwa na mama Nguruwe kwa ajili ya watoto hivyo kuwafanya wawe na afya bora itakayo wawezesha wakue haraka na kupunguza idadi ya vifo kwa watoto.

6.    Lishe bora inaongeza ufanisi wa madume ya Nguruwe na hivyo kuongeza uwezo wa kupanda

C.       Viini lishe muhimu kwenye lishe ya nguruwe

Nguruwe wanauwezo wa kula aina nyingi za vyakula lakini vyenye uwezo wa kumeng’enywa kwa urahisi. Chakula cha Nguruwe kilichokamilika kinahitaji kuwa na mchanganyiko wa viini lishe vitano, navyo ni
1.     Vyakula vyenye kutia nguvu mwilini (vyakula vyenye asili ya wanga) k.m
§    Pumba za mchele, Pumba za mahindi, Pumba za ngano, Machicha ya pombe yaliyokaushwa, Mihogo, Viazi vitamu, Viazi mviringo, Miwa, Ndizi mbichi, zilizoiva au zilizopikwa na makombo ya vyakula vya asili vya wanga n.k.
2.     Vyakula vya kujenga mwili (Vyakula vyenye asili ya protini) k.m  
§    Mashudu ya alizeti, mashudu ya pamba na mawese, unga wa dagaa/samaki, damu iliyokaushwa, soya n.k
3.     Vyakula vya asili ya madini
§    Chumvi ya mezani, chokaa ya mifugo (Limestone), mifupa iliyosagwa (bone meal), madini maalum ya nguruwe (Pig mix), madini mchanganyiko (k.m. maklic), madini ya chuma (hasa kwa watoto wa nguruwe) n.k.
4.       Vyakula vya asili ya vitamini k.m
§    Majani mabichi laini, Mbogamboga, Matunda k.m parachichi, maembe, mapapai n.k, viungo mboga kama nyanya, bilinganya n.k. Michanganyiko maalumu yenye viasilia vya vitamini k.m. Vitamini premix n.k.
5*. Maji
§    Hii ni lishe muhimu kwenye chakula cha nguruwe, ila tofauti na viini lishe vingine vilovyotajwa hapo juu ambapo nguruwe anapewa kwa vipindi/muda na kiwango maalum, maji yanahitajika kwa nguruwe muda wote. Mahitaji ya maji ya kunywa kwa nguruwe ni kama ifuatavyo:-
o   Nguruwe anayenyonyesha lita 20 kwa siku
o   Nguruwe aliyeachishwa kunyonyesha lita 5 kwa siku
o   Nguruwe wanaokuzwa na kunenepeshwa wenye kilo 20 hadi 90 lita 5 kwa siku
o   Watoto wa nguruwe lita 1 kila mmoja   

      

D.        Jinsi ya kutengeneza chakula cha nguruwe

Wakati wa kutengeneza chakula cha nguruwe inabidi kuzingatia yafuatayo:

·         Mchanganyiko wako uwe na viinilishe vinne vilivyotajwa hapo mwanzo
·        Chagua aina ya viinilishe vinavyoweza kupatikana kwa urahisi na bei nafuu kwenye mazingira yako
·     Aina ya mchanganyiko wa chakula ni muhimu uzingatie mahitaji ya nguruwe kama umri (k.m. nguruwe wanaonyonya, waliochishwa kunyonya, wanaokua, na wanaonyonyesha)
Mfano jedwali Na 1 linaonyesha michanganyiko mbalimbali ya vyakula vya nguruwe.
  1. Mchanganyiko namba 1: inapendekezwa kwa wafugaji  walioko kwenye mazingira ambayo pumba za mahindi na mashudu ya alizeti yanapatikana kwa urahisi
  2. Mchanganyiko namba 2: kwa wale ambao pumba za mahindi, za mpunga, machicha ya pombe  na mashudu ya alizeti yanapatikana kwa urahisi.
  3. Mchanganyiko namba 3: kwa wale ambao pumba  za mpunga na mahindi yanapatikana kwa urahisi.


Jedwali namba 1: Michanganyiko mbalimbali ya vyakula vya nguruwe

Na

Aina ya viinilishe

Michanganyiko

Namba 1

Namba 2

Namba 3

1

Vyakula vya wanga

 

 

 

1. Pumba za mahindi

70.25

32

30.00

2. Pumba laini za mpunga

-

25

33.00

3.  Machicha ya pombe

     yaliyokaushwa

-

21

-

4. Mahindi yaliyoparazwa

-

-

10.00

2

Vyakula vya protini

 

 

 

A. Protini ya nafaka

 

 

 

1. Mashudu ya alizeti

22.00

14

22.00

2.Mashudu ya michikichi

-

-

 

3. Soya iliyochemswa na kuparazwa

-

-

-

B. Protini ya Wanyama

 

 

 

4.Unga wa dagaa/samaki

4.00

2.00

3.25

5.Damu iliyokaushwa

-

2.25

-

3

Vyakula viasili vya madini

 

 

 

 

1. Chumvi ya mezani

0.50

0.50

0.50

 

2. Chokaa ya mifugo    

   

2.00

2.00

2.00

 

3.  Unga  wa mifupa

1.00

1.00

1.00

 

4. Madini na vitamini    

    mchanganyiko

0.25

0.25

0.25

 

         Jumla

100.

100

100.



E.     Kiasi na namna ya kulisha

·         Nguruwe wanahitajika kulishwa aina hii ya chakula mara mbili (asubuhi na mchana) au zaidi kwa siku
·         Kiwango/kiasi cha kulisha kwa nguruwe wa aina na rika tofauti kimeonyeshwa kwenye jedwali Namba 2
·         Pamoja na vyakula vilivyotajwa, wafugaji wanashauriwa kuwapatia nguruwe vyakula vyao vya asili kama vyakula vya ziada mfano, majani mabichi laini, majani ya maboga, mbogamboga, matunda kama maparachichi, majani ya viazi n.k.     

Jedwali na 2:  Viwango vya kulisha Nguruwe wa uzito mbalimbali

Na
Wakati
Uzito wa nguruwe (kilo)
kiasi cha chakula  (kilo kwa siku)
1.
Baada ya kuachishwa kunyonya hadi uzito kiasi
10 - 17
0.75
2.
Uzito uliozidi kiasi kidogo
18 - 29
1.00
3.
Uzito wa kawaida
30 - 40
1.50
4.
Uzito mkubwa kiasi
41 - 60
2.00
5.
Uzito mkubwa
61 - 80
2.5
6.
Uzito mkubwa sana
81 - 100
3.00
Jinsi ya kulisha makundi mbalimbali ya nguruwe
1.        Kipindi cha mamba, kuzaa hadi kuachisha kunyoyesha
1.1 Kipindi cha miezi mitatu baada ya kupandishwa
·              Apatiwe chakula kiasi k.m. kilo mbili kwa siku
·              Kiasi hiki kiendelee hadi wiki 3 kabla ya kuzaa
1.2 Wiki tatu kabla ya kuzaa
·              Ongeza chakula kufikia kilo 2½.
1.3 Wiki moja kabla ya kuzaa
·              Anza kuopunguza chakula taratibu hasa vyakula vya nafaka (Concentrate rations).
·              Ongeza vyakula vya  mbogamboga, majani laini na matunda (laxative meals).
1.4 Siku ya kuzaa
·              Usimpe chakula chochote cha nafaka.
·              Mpe vyakula vya mbogamboga,na  vilaini kwa kiasi kidogo tu
·              Mpatie maji ya kutosha.
1.5 Siku ya 1 – 2 baada ya kuzaa
·              Mpe ½ kilo ya chakula kamilifu.
1.6 Siku ya 3 na kuendelea
·              Ongeza chakula cha nafaka kwa kiasi cha kilo 1 kwa siku.
·              Ongeza kufikia kiwango kinachohitajika kulingana na idadi ya watoto alionao mama nguruwe.

Zingatia

·              Mama nguruwe anahitaji kilo 3 za chakula kwa matumizi yake ya kawaida.
·              Atahitaji kiasi cha theluthi moja (1/3)  ya kilo ya chakula kwa kila mtoto aliyenae
Mfano: kama mama ana watoto 9 atahitaji kiasi gani cha chakula?
Mahitaji mama peke yake
Mahitaji kutokana na watoto
Kiasi cha chakula kwa siku
3kg
Theluthi moja x 9
Kilo 6 kwa siku
                  3     +         (1/3   x  9)       =      6 Kg
·              Endelea kumpa kiwango hicho cha chakula mpaka ifikapo wiki moja kabla ya kuwaachisha watoto kunyonya.
·              Wiki moja kabla ya kuwachisha punguza kiwango taratibu mpaka kufikia kilo 3½ kwa siku.
 
Baada ya kuachisha kunyonya
·              Mama nguruwe apatiwe chakula bora kilicho na kiwango kikubwa cha madini na vitamini  kiwango cha kilo 2 – 3 kwa siku.
·              Hii itamsaidia kuivisha mayai, hivyo kumsaidia kupata joto mapema.

Chakula kwa ajili ya watoto wa nguruwe (Creep feed)
§    Hiki ni chakula wapewacho nguruwe wachanga wakiwa na umri wa wiki ya pili hadi wiki ya tatu.
§    Kipindi hiki mahitaji ya watoto ni makubwa ambayo hayawezi kuteshelezwa na maziwa pekee ya mama yao.
§    Chakula hiki kitawasaidia watoto kuzoea chakula kigumu, kutosheleza mahitaji yao, na hivyo huwawezesha watoto kukua kwa haraka
§    Creep feed inaweza kutengenezwa kwa kuchanganya viini lishe vifuatavyo

Aina ya  viinilishe
Asilimia
Mahindi yaliyobarazwa
30
Pumba za mahindi
40
Mashudu ya alizeti
18
Unga wa Dagaa
10
Unga  wa mifupa
0.5
Chokaa ya mifugo (limestone)
0.75
Chumvi ya mezani
0.5
Premix
0.25
Jumla
100

Fahamu mbinu za kuongeza thamani nyama

  Safari ya kuongeza thamani nyama ya mifugo huanzia shambani kwa usimamizi wa ufugaji na uzalishaji. Lishe bora ni muhimu kwa wa ufugaji ...