MRADI WA UFUGAJI SUNGURA KIBIASHARA.

 

KIBANDA CHA KUFUGIA
Tunasaidia kwenye ujenzi wa vibanda bora vya sungura,  kwagharama ya Tshs 65,000/=  tu    kwa kimoja cha  ukubwa  wa  futi 2.53  ,  chenye  uwezo  wa  kufugia  Sungura  mmoja  mkubwa  wakuzalisha  pamoja  na watoto wake kwa mwezi mmoja baada yakuzaliwa yaani kipindi chote cha unyonyeshwaji, na kibanda cha saizi hiyo pia kinaweza kufugia hadi sungura kumi wa umri wa miezi mitatu.
Tunashauri ujenzi wa vibanda vitatu kwa kila jike (kupata nafasi ya watoto wanaomaliza kunyonya kwani jike huzaa kila baada ya miezi 2) na pia kibanda kimoja kwa kila dume.

MBEGU
Tunawataka wakulima wetu kufuga mbegu bora na halisi ya sungura watakaotupa nyama bora kwa soko letu,  na  tunawauzia  kwa  gharama  ya  Tshs  80,000/=  kwa  kila  jike  aliyetayari  kubeba  mimba   na  Tshs 40,000/= kwa kila dume mwenye umri wakuzalisha.

MAFUNZO YETU
Tuna  mafunzo  mara  kwa  mara  pia,  na  zaidi  kuhusu  ujezi  wa  mabanda  bora,  Utunzaji  na  ufugaji  kwa ujumla, na kuhusiana na maswala ya magonjwa na namna yakuzuia.
Tuna  saini  mkataba na mkulima/mfugaji  (kwa  ada  maalum  kila  mwaka)  ambao utamuhakikishia mfugaji/mkulima  soko kwa kipindi chote cha mkataba  pale sungura wake wanapokuwa tayari kwa kuuzwa.
Tunanunua sungura katika umri wa miezi 4-5. Kwa umri huo sungura mwenye afya aliyelishwa vizuri anapaswa kuwa na uzito wa kilo 3-4, na kilo moja ya sungura akiwa hai tunamnunua kwa Tshs 8,000/=.

Tafadhali wasiliana nasi kwa maelezo zaidi.
http://mkulimajembemfugaji.blogspot.com/p/ontact.html
Tafadhali zingatia mafunzo kwa mtunzaji wa sungura wako/au kama ni wewe mwenyewe ni ya muhimu kujifunza mambo ya msingi unapoanza mradi nasi,
Paleunapohitaji ushauri wa kitaalam utagharimia nauli ya mtaalamu atakufundisha UFUGAJI BORA WAKISASA kwa vitendo.

Comments

Post a Comment

Popular Posts