Kilimo cha Kisasa cha Mahindi
"Kulingana na msimu mahindi hupandwa mwanzoni mwa mwezi wa 11 baada ya mvua za kwanza kunyesha (specifically from 1st to 15th day of November) ambayo huvunwa mwezi Machi mwishoni au aprili mwanzoni. Pia mahindi hupandwa mwanzoni mwa mvua za masika yaani mwezi wa pili mwishoni na mwezi wa tatu mwanzoni ambayo huvunwa mwezi Julai katikati na Agosti mwanzoni...."
KUANDAA SHAMBA, KUPANDA NA
KUPALILIA
1. Kuandaa Shamba, Kusafisha, Kulima/Kutifua
Ni vyema mashamba yaandaliwe
mapema kabla ya msimu wa kupanda haujaanza ili kumpa mkulima fursa ya kupanda
kwa wakati unaotakiwa.
Kuna njia mbalimbali
zinazotumika kuandaa mashamba. Kati ya njia hizi ni pamoja na kufyeka, kung’oa
visiki na kulima. Shamba linaweza kulimwa kwa kutumia:
i). Jembe la mkono - wengi wanatumia
ii). Jembe la kukokotwa na wanyama kama ng’ombe
iii). Power tillers
iv). Matrekta
Matumizi ya trekta, power
tillers na jembe la kukokotwa na
wanyama yanapunguza nguvu kazi kwani vinachimbua udongo na kuufanya kuwa
tifutifu (kufanya isiwe na mabonge makubwa, wala isiwe vumbi vumbi). Hii
husaidia:
i). Mizizi ya mimea kupenyeza ardhini kirahisi
ii). Udongo kuweza kuhifadhi maji
iii). Udongo kuwa na hewa inayohitajika na mimea
iv). Ukuaji mzuri wa mimea hivyo kuongeza mavuno
2. Kupanda
Mbegu Bora
Matumizi ya mbegu bora ni
muhimu katika upatikanaji wa mavuno mengi na bora. Kuna makundi mawili makuu ya
mbegu ambayo ni:
i). Mbegu za asili: Ni zile ambazo zimetumika
miaka mingi katika historia ya kilimo
ii). Mbegu zilizoboreshwa: Hizi ni zile zilizoboreshwa
kutoka mbegu za asili. Kundi hili linagawanywa kwenye makundi mawili - composite
varieties na mbegu
chotara (Hybrids).
Ushauri wa matumizi ya mbegu
zilizoboreshwa unatofautiana kutoka eneo moja na lingine kwa sababu ya:
i). Mwinuko kutoka usawa wa bahari
ii). Kiasi cha mvua katika eneo husika
iii). Muda unaotumia mbegu hadi kukomaa
Mbegu za mahindi
zilizoboreshwa ni kama TMV1, TAN 250, TAN 254, Staha, Situka na zingine zote zinazoanza
na herufi “H” kama vile H 250, H 251 na H
615.
Pia mbegu
mpya zilizotangawa na Kamati ya Taifa ya Mbegu mwaka huu ni
·
WE4102 · WE4106 · WE4110
·
WE4114 · WE4115
kutoka ARI ILONGA.
Jinsi Ya Kuweka Mbolea Za Kupandia
Mbolea hizi zinawekwa
shambani kabla ya kupanda/kusia mbegu. Zinawekwa kwa njia mbalimbali kama vile
kusambaza kwenye eneo husika na kuchanganya na udongo, au kuweka kwenye mistari
au mashimo ya kupandia. Ni bora zaidi kuchanganya mbolea za Minjigu Phosphate
au Minjingu Mazao na udongo kuliko kutia kwenye shimo la kupandia. Pia
kuchanganya mbolea na udongo huondoa athari za mbolea kwenye uotaji wa mbegu,
hasa kama kuna uhaba wa unyevunyevu.
Viwango Vya Mbolea Za Kupandia
Kiwango cha mbolea za
kupandia kilichopendekezwa ni kilo 20 fosfati (P) kwa hektari ambayo ni
sawasawa na kiasi cha aina mbambali za mbolea za kupandia kama inavyoonyeshwa
kwenye jedwali namba 1.
Jedwali na. 1: Kiasi cha
mbolea za kupandia kwa inayopendekezwa kwa eneo (hektari au ekari)
Aina
ya mbolea za
kupandia
|
Idadi
ya mifuko ya kilo 50 kwa hektari
|
Idadi
ya mifuko ya kilo 50 kwa ekari
|
Viwango
kwa kila shimo
|
DAP
|
2
|
1
|
Nusu kizibo cha soda
|
Minjingu fosfati
|
3
|
1½
|
Kizibo kimoja cha soda
|
Minjingu Mazao
|
4½
|
2
|
Kizibo kimoja na nusu cha
soda
|
Muda
wa kupanda
Kulingana
na msimu mahindi hupandwa mwanzonimwa mwezi wa 11 baada ya mvua za kwanza
kunyesha (specifically from 1st to 15th day of November)
ambayo huvunwa mwezi Machi mwishoni au aprili mwanzoni. Pia mahindi hupandwa mwanzoni
mwa mvua za masika yaani mwezi wa pili mwishoni na mwezi wa tatu mwanzoni ambayo
huvunwa mwezi Julai katikati na Agosti mwanzoni. Katika msimu huu utayarishaji
wa shamba hufanyika mwezi wa pili mwanzoni.
Muda wa kupanda
unatofautiana kutoka eneo moja kwenda jingine kulingana na majira ya mvua. Kwa
mfano katika wilaya ya Morogoro tarehe za kupanda ni kuanzia februari 15 hadi
Machi 15. Mkulima anashauriwa afuate kalenda ya muda wa kupanda kama
anavyoshauriwa na bwana shamba wake.
Kupanda
kwa nafasi
Kupanda kwa nafasi ni kati
ya njia bora za kilimo inayomwezesha mkulima kupata mazao bora. Hivyo ni muhimu
sana kuzingatia kupanda kwa mistari na kufuata nafasi zinazoshauriwa na
wataalamu wa kilimo. Kwa mfano nafasi zifuatazo zinaweza kutumika katika
upandaji wa mahindi:
Nafasi
|
Idadi ya mbegu kwa kila shimo
|
Kiwango cha mbolea kutumia kizibo cha chupa
|
90 sm X 30 sm
|
1
|
1
|
90 sm X 25 sm
|
1
|
1
|
90 sm X 50 sm
|
2
|
2
|
3. Kupalilia
Ni muhimu shamba lipaliliwe
baada ya mimea kuota ili kuondoa magugu. Magugu ni mimea hivyo hushindana na
mimea iliyopandwa na mkulima kwa kunyonya virutubisho ardhini. Magugu yanaweza
pia kuhifadhi wadudu na magonjwa yanayoweza kushambulia mimea iliyopandwa na
hivyo kupunguza mavuno. Magugu yaweza kuondolewa wa palizi ya mkono (yaani)
kung’olea (ikiwa magugu yapo mbali mbali sana) au kulima kwa jembe la mkono au
kwa kutumia dawa/viuagugu (HERBCIDES) hasa 2-4D.
Mbolea
za kukuzia
Ni mbolea zinazotumika baada
ya mimea kuota kwa lengo la kuikuza mimea ili itoe mavuno bora. Mara nyingi
mbolea hizi zinatoa kirutubisho cha naitrojeni. Mbolea maarufu za kukuzia
katika soko la Tanzania ni kama:
AIna ya mbolea
|
Kiwango cha kirutubisho cha naitrojeni
|
Urea
|
46%
|
Calcium Ammonium Nitrate
(CAN)
|
23%
|
Sulphate of Ammonia (SA)
|
21%
|
Urea inakirutubisho cha naitrojeni (N) kwa kiwango
kikubwa na watu wengi wanauzoefu nayo. Vilevile bei yake ni nafuu
ikilinganishwa na mbolea zingine za kukuzia. Mbolea hii iko katika hali ya
chengachenga za mviringo (granules)
za rangi nyeupe. Kiwango
cha urea ni nusu kizibo cha soda kwa kila shina. Mbolea hizi hazidumu kwenye
udongo kwa muda mrefu kwa hiyo huwekwa shambani wakati mimea inapokuwa na
mahitaji makubwa ya kirutubisho cha naitrojeni na wakati udongo una unyevunyevu
na shamba halina magugu.
Pia wakulima hutumia mbolea za
kukuzia zinazopatikana kwa bei nafuu kama vile BOOSTER (foliage nitrogeneous
fertilizers) ambayo hupigwa kwa kunyunyizia katika majani ya mmea kila baada ya
wiki 3, kwa mara 2-3 mpaka mahindi kuvunwa. Kiwango cha kupiga ni mchanganyo wa
mls 50-80 ktk lita 15 za maji. Mbolea
za kukuzia huwekwa kuzunguka kila shina la mimea au pande mbili au tatu au nne
za kila shina. Cha muhimu ni kwamba mbolea isirundikwe sehemu mmoja. Minjingu
Mazao (kg50/ekari = gramu 10kwa shimo) pia yaweza tumika kwa kukuzia, hivyo
mkulima yko huru kuchagua kulingana na uwezo na upatikanaji wake.
Viwango
Vya Mbolea Za Kukuzia Vinavyoshauriwa
Kiwango kinachopendekezwa ni
kilo 60 naitrogeni kwa hektari, ambacho ni sawasawa na kiasi kama
inavyoonyeshwa kwenye jedwali namba 2. Mbolea inayotumika mara kwa mara ni
Urea. Hata hivyo mbolea zingine kama SA inaweza kutumika kama kuna mahitaji ya
salfa. CAN inaweza kutumika kama kuna mahitaji maalum ya nitrate
na ammonium.
Kwenye mahindi mbolea ya
kukuzia inawekwa baada ya palizi ya kwanza ambayo ni kama wiki tatu mpaka wiki
nne baada ya kupanda.
Jedwali na. 2: Kiasi cha
mbolea za kukuzia kwa inayopendekezwa kwa eneo (hektari au ekari)
Aina ya mbolea za kukuzia
|
Idadi ya mifuko ya kilo 50 kwa hektari
|
Idadi ya mifuko ya kilo 50 kwa ekari
|
Viwango
|
Urea
|
2
|
1
|
Nusu kizibo cha soda
|
CAN
|
4½
|
2
|
Kizibo kimoja cha soda
|
SA*
|
3
|
1
|
Nusu kizibo cha soda
|
Mambo
Muhimu Ya Kuzingatia
Kuweka mbolea:
Sehemu za nchi ambazo muda
wa kukua mahindi ni mrefu (zaidi ya miezi mitatu), ni vyema kuweka mbolea za
kukuzia mara mbili, yaani nusu ya kiwango kinachopendekezwa baada ya mwezi
mmoja, na kurudia tena (kutumia nusu iliyosalia) baada ya wiki tatu.
Kupalilia:
Katika kilimo cha mahindi,
ni muhimu shamba lipaliliwe siku 14 hadi 21 baada ya mimea kuota kufuatana na
hali ya shamba wakati wa kupanda. Wataalamu wanashauri kwamba katika kilimo cha
mahindi, shamba lipaliliwe mara 2-3, kufuatana na hali ya magugu katika shamba.
- Utafiti unaonyesha kwamba,
shamba la mahindi ambalo halijapaliliwa linaweza kupunguza mavuno kwa asilimia
60 hadi 100 ya mavuno yanayotarajiwa. Hata kama mkulima atatumia mbegu bora,
aina na kiasi cha mbolea zinazoshauriwa, kupanda kwa mstari pamoja na mbinu
nyingine bora zinazoshauriwa, bila kupalilia hali hii itaathiri mavuno yake.
KUDHIBITI MAGONJWA NA WADUDU
WANAOSHAMBULIA MAHINDI
Magonjwa Yanayoshambulia
Mahindi
i)
Maize streak virus
Dawa/Kudhibiti:
Mbegu bora inayostahimili
ugonjwa, kupanda mapema, kung’oa mimea iliyoathirika ama kunyunyiza dawa za
kuua ‘vectors’
kama vile inzi weupe (white
flies).
ii)
Smut (Fugwe)
Dawa/Kudhibiti:
Tumia Helerat
ukifuata maagizo kamili.
iii)
Cob rot (kuoza kwa mhindi)
Dawa/Kudhibiti:
Tumia mbegu zinazostahimili
kuoza.
Wadudu Na Wanyama
Wanaoshambulia Mahindi
a)
Viwavi Jeshi
Ni wadudu aina ya
funza ambao hutokana na Nondo.Hushambulia mahindi kwa kula majaniyake pamoja na
shina. Wadudu hawa huangamizwa/kudhibitiwa kwa njia zifuatazo;-
- Kuondoa vichaka karibu na shamba
- Kunyunyizia sumu za asili kama vile Mwarobaini majuma mawili ya mwanzo.
- Kunyunyizia sumu za viwandani endapo wadudu wameanza kuonekana kama vile Karate 1ml/1l
b)
Funza wa Mabua (Maize Stalk Borer).
- Funza wa mabua hutoboa shina la mahindi na kusababisha kudumaa kwa mahindi.
- Matundu, ungaunga kama wa msumeno huonekana kwenye majani yaliyoathiriwa.
- Mashambulizi huanza juma la pili hadi la tatu baada ya mahindi kuota.
Njia
za kudhibiti zinazotumika
- Kuchanganya mahindi na mazao jamii ya mikunde km vile maharagwe
- Kung’oa mahindi yaliyoshambuliwa
- Sumu za asili mwarobaini
- Sumu za viwandani km vile Karate. pia waweza tumia Malathion, sumithion, vumbi ya cymbush au Sevin 5G na ufuate maagizo kamili.
c)
Cutworms (Vikata Shina)
Dawa/Kudhibiti: Tumia Dragnet FT na ufuate maagizo kamili.
d)
Wanyama waharibifu
Kudhibiti:
Kuwatishia na kuwafukuza
wanyama.
Ili mkulima aweze kupata
mazao mengi na bora inashauriwa kutumia dawa za kuzuia magonjwa na wadudu
washambuliao mimea na njia zinginezo.
KUVUNA,
KUKAUSHA, KUSAFISHA NA KUHIFADIHI
Kuvuna
Mahindi yako tayari kuvuna wakati kikonyo kimekuwa
dhaifu na mahindi yanaangalia chini. Mahindi yakishakauka vizuri
yanatenganishwa na bua halafu majani ya mhindi kutolewa.
Kukausha
Kama mahindi hayajakauka vizuri hukaushwa zaidi
katika juani siku 3-4 ili kupunguza unyevunyevu kufikia kiwango kinachofaa kwa
kuhifadhi (14%). Ni muhimu mahindi yakauke vizuri ili yasioze yakiwekwa
ghalani.
Ili kujua kama mahindi yamekauka vizuri, tia mahindi kadhaa kwenye chupa ya soda iliyokauka na uongeze kiganja kimoja cha chumvi. Tingisha chupa halafu uwache itulie kwa dakika tatu. Chumvi ikikwama kando ya chupa, basi mahindi hayajakauka vizuri.
Kusafisha
Mahindi yaliyokauka vizuri hupepetwa na vilevile
mahindi mabovu huondolewa.
Kuhifadhi
Mahindi
huhifadhiwa ghalani baada ya kuwekwa viatilifu vya kuzuia bungua wa mahindi
Njia za kisasa za uhifadhi hutumiwa kama vile matumiz ya ACTELLIC SUPER DUST
katika uwiano wa 1kg kwa gunia 5-10 za ujazo wa 100kg. Kiatilifu kingine ni
actellic solution katika rate ya 5mls katika gunia moja la kg 100.
Njia
nyingine ya kienyeji katika kuhifadhi mahindi ni kuweka juu ya ghala ambalo
chini yake kuna jiko la kupikia ambalo hutoa moshi unaotumika kufukuza na kuua
wadudu.
Comments
Post a Comment