KILIMO BORA CHA MIWA

KILIMO BORA CHA MIWA
KILIMO BORA CHA MIWA
KILIMO BORA CHA MIWA : Kilimo cha miwa ni kilimo chenye tija kwa mkulima, kilimo hiki kinaweza kufanywa na mtu yeyote yule aidha awe ameajieiwa au laaa! Jambo la msingi ni kuhakikisha anajitoa kikamilifu katika kuhakikisha  unawekeza akili yake katika kulima kilimo hiki.
Kuna aina kuu 2 za miwa katika mbegu za miwa zilizo shamili sana ambazo ni:
  1. Bungala
  2. Miwa myekundu.
Unachotakiwa kufanya katika kulima kilimo hiki ni, Kwanza kabisa tafuta ekari moja ya shamba kisha anza maandalizi lakini zingatia kupuguza matumizi makubwa ya pesa kadri iwezakanavyo yaani kwa shughuli nyinginezo ambazo unaweza kuzifanya mwenyewe ni vyema ukazifanya ili kupunguza matumizi makubwa ya pesa mfano kulima, kupiga dawa, kupalia n.k
Tafuta mbegu ya miwa ya Bungala miwa hii ni laini sana na ni rahisi kuichana kwa kutumia meno, baada ya kupata miwa hii kata vipande vipande vya pingili tatu tatu .Kumbuka kwamba miwa ni rahisi sana kushambuliwa na mchwa pale tu inapokuwa imepandwa.

Ili kuzuia isiliwe na mchwa nenda katika maduka ya kilimo na ununue moja wapo ya madawa yafuatayo:-
  1. TAP 4% GR Tumia gram 100 za dawa kwa lita takribani 20 za maji kisha nyunyizia katika mashina ya miwa.
  2. Taniprid 25 WG. Tumia gram 100 za dawa kwa lita takribani 20 za maji au pia unaweza kuweka kijiko kimoja cha chai katika kila shina.
  3. Imida Gold Mls 20 kwa lita 20 za maji na unyunyizie shinani.
  4. Gammalin 20. Tumia gram 100 kwa lita takribani 20 za maji. Na unyunyizie katika vipande vya miwa au chovya vipande vya miwa katika maji hayo yaliyo na Gammalin 20 na ndipo uende ukavipande shambani kwako.
  5. Gladiator FT.
  6. Stom

Mambo yakufanya:
Zingatia kama utatumia aidha Gladiator au Gammalin au Stom, chukua ndoo ya maji ya lita 20 kisha uichanganye na dawa uliyoinunua kisha chukua kipande cha muwa na kukizamisha ndani ya maji hayo na baadae uende kuipanda shambani kwako, hivyo uewezekano wa miwa yako yote kuote utakuwa ni mkubwa sana maana shida kubwa ni mchwa na hapo tayari utakuwa umeidhibiti.

UPANDAJI WA MIWA
Hakikisha unapokuwa unapande miwa yako acha nafasi ya mita moja (1m) kati ya mche na mche pia hakikisha una acha nafasi ya mita moja (1m) kati ya mstari na mstari. Kumbuka awali tulisema katakata muwa wako kupata vipande vilivyo na vipingili vitatu vitatu, hivyo sasa unapokuwa unapande miwa hii hakikisha hizo pingili zote 3 zimezama ndani ya ardhi na kipande kidogo tu ndio kibakie juu ya uso wa ardhi na mche wako huo unapoutumbukiza kwenye ardhi uwe umelala wastani wa nyuzi 30.

Zile pingili katika muwa wako kumbuka ndipo sehemu hasa miwa inamokuwa inachipuka na kuota. Mantiki ya kuacha nafasi kubwa kati ya mche na mche ni kwa sababu hilo shina lako moja ulilolipanda linaweza likachipua vijimiwa vingine zaidi hata ya ishirini kama ukiliacha shina liendelee kuzaa tu kwa kadri linavyotaka na hatimaye shamba lako litakuwa msitu hata usiopitika.

Lakini kibaya zaidi ni kwamba miwa yako itakosa afya njema na mwisho wa siku miwa yako haitakuwa bora hata bei haitakuwa nzuri pindi utakapoamua au wakati wa kuuza utakapofika. Hivyo unashauriwa kuacha miwa kati ya tano mpaka kumi lakini mfano ukiacha miwa mitano katika shina moja ni dhairi hewa na mwanga vitakuwa vya kutosha shambani lakini hata chakula na virutubisho vingine kwa miwa hiyo vitakuwa lukuki na sio vya kung’ang’aniana hivyo mwisho wa siku utapata miwa mirefu na minene ambayo sokoni itakuwa na mvuto mkubwa kwa wateja.

Mfano chukulia kwamba umelima ploti ndogo tu ya upana mita 50 kwa urefu mita 70, kumbukumbu namna ya upandaji miwa kama tulivyozungumza hapo awali umbali wa mita moja moja kwa kila shina. Hivyo kwa ploti ya shamba hili utakuwa na miche au mashina uliyopanda kiasi cha 70×50=3500 (mashina elfu tatu na mia tano) sasa chukulia kwa hesabu rahisi kwamba kila shina umeruhusu miwa mitano tu ndio ikuwe pale maana yake kwa mashina 3500 utazidisha mara 5 ambapo itakuwa 3500×5= 17,500 hiyo ndio itakuwa jumla ya miwa itakayovunwa shambani.

Kwa tafiti zilizofanywa zinaonesha kama hautaki shida na unahitaji pesa ya haraka haraka sana huko huko shamba, basi unaweza ukajumlisha miwa yako kwa bei ya chini sana yaani tukadilie vile kwamba tunahitaji pesa ya haraka so tuuze muwa mmoja kwa bei ya jumla ya 300 hivyo jumla ya pesa utakayoipata itakuwa 17,500 × 300 = 5,250,000 (milioni tano laki mbili na nusu). Hiyo ni pesa ya haraka haraka huko huko shambani .

Ila kama ukiweza kusogea zaidi na kuuza kwa faida maana kama umeweza kupigana mpaka kuweza kuikuza ni dhairi kwamba unastahili kupata faida iliyo njema kwako hivyo ni muhimu kuangalia masoko yamekaaje pande zote za miji, ila kama utaweza kuifikisha Dar es Salaam ambako kiuhalisia soko lake ni kubwa sana .

Kama ukienda Kariakoo bei ya rejareja kwa muwa aina ya bungala wenye wastani wa urefu mita moja na robo bei yake ni 5,000 lakini ukienda mtaani kwa muwa huo huo aina ya bungala mfupi kidogo bei yake inakwenda mpaka 3,500 hivyo chukulia kwamba umeweza kufikisha Dar es Salaam huo mzigo wako wa miwa, hivyo mapato yako kama utaamua uuze kwa bei ya jumla ya 1,500 kwa kila muwa hivyo kiasi cha fedha utakachokipata kitakuwa ni sawa na idadi ya miwa yako zidisha bei ya kujumlishia yaani ingekuwa 17,500 × 1,500= 26,250,000 hii ni pesa utayoipata kwa halali kabisa wala haujamzulumu mtu.

Hapo umelima ploti ndogo tu, sasa chukua pengine umelima ekari moja na kwa shamba la miwa ekari moja kiwango cha chini kabisa cha wewe kuvuma miwa yako ni jumla ya miwa 24,500. Sasa chukulia kama umeweza kuipeleka Dar es Salaam maana yake utapata jumla ya 24,500 × 1,500= 36,750,000. Sasa mfano ndo ukalima ekari 4 hadi 5 hapo ni hakika unatoka katika kundi la uchumi wa chini na kuingia katika uchumi wa kati. Jamani bado hatujachelewa kungali bado fursa ziko kinachohitajika hapa ni kuthubutu tu, Mungu akubariki unapoyatafari haya lakini pia pindi ukifanikiwa usimsahau Mungu maana yeye ndiye nguzo ya mafanikio yako yote.
MIWA
MIWA

Comments

  1. Je hekari moja ya shamba la miwa linahitaji mbegu kiasi gani .naomba unisaidie kujua gharama za mbegu tafadhali ,

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular Posts