Aina za Pilipili
- Pilipili kali (Bird’s eye / kichaa)
- Pilipili hoho (Bell pepper)
- Pilipili ndefu (Cayenne)
Hatua za Kilimo
Uchaguzi wa Mbegu
- Tumia mbegu bora zilizoidhinishwa.
- Chagua aina inayohitajika sokoni (kwa export au soko la ndani).
Kuandaa Kitalu
- Panda mbegu kwenye kitalu chenye kivuli.
- Mwagilia kila siku.
- Miche huwa tayari kupandikizwa baada ya siku 21–30.
Maandalizi ya Shamba
- Udongo tifutifu unaopitisha maji vizuri.
- Ongeza samadi au mboji.
- Nafasi: cm 45–60 kati ya mistari na mimea.
Kupandikiza
- Fanya asubuhi au jioni.
- Mwagilia mara baada ya kupandikiza.
Matunzo
- Palilia mara kwa mara.
- Weka mbolea (NPK mwanzoni, CAN au Urea baadaye).
- Dhibiti wadudu (vidukari, thrips) na magonjwa (ukungu).
Uvunaji
- Huanza siku 75–90 baada ya kupandikiza.
- Vuna mara 2–3 kwa wiki.
- Kwa export, chagua pilipili zenye ubora na zisizo na doa.
Soko na Faida
- Soko la ndani: masoko ya mijini, hoteli, viwanda vya chakula.
- Soko la nje: Kenya, Ulaya, Mashariki ya Kati (hasa pilipili kali).
- Bei hupanda kipindi cha kiangazi.
Faida za Kiafya
- Ina Vitamin C nyingi.
- Husaidia kuongeza kinga ya mwili.
- Huchochea mmeng’enyo wa chakula.
Unahitaji Makadirio ya gharama na faida kwa ekari moja pamoja na mbinu za kupata soko la uhakika.wasiliana na Mkula Jembe +255756483174



No comments:
Post a Comment